MAFUNZO MAALUM: JINSI YA KUFANYA WAZO LIWE BIDHAA INAYOLIPA

Je una wazo la biashara ila haujui unaanzaje kulifanya liwe kweli ni bidhaa ? Je umekua ukibuni bidhaa Fulani Fulani ila haupati “bahati” ya kufikia wateja wengi na kufaidika na bidhaa yako ? Basi jibu lipo katika uwezo sahihi wa kuunda bidhaa kwa kitaalamu tunaita Product Development.

Ni kweli kuwa fursa zipo nyingi sana na kinachotakiwa ni umakini wa kuziona. Ili uzione fursa wakati mwingine inakupasa uwe tayari una taarifa nyingi nyingi kuhusiana na uwezekano wa kufanya jambo fulani, kwani kwa hayo mambo ambayo unayajua ndio utaweza tambua kitu kinachowezekana kufanyika wakati watu wengine wanaona haiwezekani, wakati wengine wanaona ni matatizo , wewe unajiumia kichwa kujua suluhu yake itakuaje.

Kuna namna nyingi ambapo "ideas" huja, na sio kila idea inaweza kukuingizia fedha. Ukishapata idea itakupasa ujue namna ya kuichambua, namna ya kutengeneza thamani kweli kweli ili walengwa wainunue, na namna ya kupangilia vile utakavyoiwasilsha bidhaa au huduma yako uliyoweza itengeneza kupitia "idea" yako.
Mchakato woote huu kitaalamu tunauita PRODUCT DEVELOPMENT. Na ijumaa hii March 3, 2017 kupitia WhatsApp group na FB groups maalum, nitaelezea mbinu mbalimbali tunazotumia ktk kubuni na kuunda bidhaa toka kwenye idea mpaka kitu kinachoeleweka na kuuzika.
Haijalishi ni idea ya kuwa na app, idea ya kuuza bidhaa fulani, au kutengeneza bidhaa fulani, yote tuyajadili kwa umakini. Utajifunza namna ya kutafiti soko, namna ya kuunda VALUE kwa bidhaa yako, na mbinu za kujaribu haraka haraka bidhaa yako. Pia utapata ufafanuzi kuhusu namna ya kuwafikia wateja ili waweze nunua bidhaa zako.


Wasiliana nami kwa WhatsApp +57 301 297 1724 au +255 757 120 020 tukupe utaratibu wa kujiunga ktk somo hili la siku moja tuu. 
Share:

0 comments:

Post a Comment