JIFUNZE ENGLISH: JINSI YA KUTOA MAELEKEZO AU AMRI KATIKA ENGLISH

Katika mawasiliano ya English ni muhimu kujua kuongea kwa namna sahihi hivyo basi ndio maana katika somo hili utaangalia namna ya kuandika na kuongea sentensi ambazo ni za kutoa maelekezo au tuseme kuamrisha. Sentensi hizi kwa English huitwa imperatives au command.

Jinsi ya kuunda sentensi ya kuamrisha/kutoa maelekezo katika English
Sentensi zote za kuamrisha katika English zinafuata kanuni kuu mbili :
Kwanza huwa na verbs zenye infinitive,
Yaani matendo yanayotajwa huandikwa au kusemwa bila kuyabadilisha vyovyote vile mfano tunajua kula ni EAT , basi utataja hivyo hivyo EAT bila kuanza kufikiria kwa namna gani ubadilishe nyakati ya hiyo verb husika.
Mfano mwingine tukio la kulala ni  SLEEP basi utatumia hilo hilo neno sleep bila kujiuliza ni kwa namna gani utabadili.
Pili daima kumbuka sentensi huwa zinaelekwa kwa nafsi ya pili
Yaani kwakua ni amri basi anayepokea  hiyo amri ni WEWE au NINYI kwa English tunasema YOU.
Hivyo basi ndio maana tunasema:
Sit down !  - Kaa chini  ( Yaani wewe au ninyi kaeni chini).
Go ! - Nenda ( Yaani wewe nenda au ninyi neneni)
Get out ! ( Yaani wewe toka au ninyi tokeni)

Kwanini uzingatie kuelewa jinsi kuamrisha na kutoa maelekezo kulivyo katika English
Ni kwa sababu wakati mwingine kama utatumia sentensi za namna hii bila kukusudia kutoa amri au maelekezo utajikuta ukieleweka vibaya. Hivyo kwa mfano kama unataka kuomba kitu au kupatiwa ufafanuzi fulani usiandike sentensi yako kiasi kwamba ikaonekana ni kama vile ni amri.
Na wajua wazi kama unataka kuomba kitu halafu ikaonekana kwa sababu ya ongea yako kuwa ni kama una amrisha, haitojenga picha nzuri na hivyo hutopewa unachotaka.

Namna ya kutoa amri au maelekezo ila usionekane unafanya kwa ukali
Ili usionekane mkali katika kitu unachotaka mtu afanye tumie neno please, can, could au would.
Mfano:
Please don’t come here badala ya  Don’t come here !
Would you sit down  ? Badala ya Sit down !
Can you come here ? Badala ya Come here !
Pia waweza tumia sentensi fupi kabla ya kutoa maelekezo. Sentensi zenyewe ni kama vile:
Would you mind….,  Would you please….,  I was wondering if  you can …..,
Mfano: Would you mind  to sit down ?  I was wondering if you can go .

Hitimisho:
Ni muhimu sana kujua kanuni na jinsi ya kuongea vizuri English. Tatizo la kutokufuata kanuni na miongozo ya English ni kuwa utajikuta unachoelezea kikaeleweka tofauti.
Kwa maelekezo zaidi ya English ingia kwa group letu la WhatsApp la JifunzeEnglish, kwa kutuma maombi yako kwa namba +57 301 2971724 au +255 757 120 020. Jitambulishe na useme unahitaji kusaidiwa nini.
Share:

0 comments:

Post a Comment