KANUNI MUHIMU KUHUSU PERSONAL PRONOUNS

personal pronouns rules
Personal pronouns kwa Kiswahili Viwakilishi vya nafsi, ni maneno yanayotumika badala ya kutaja majina ya watu, vitu, maeneo, hali n.k
Mfano : Badala ya kusema John and Juma are happy. (John na Juma ni wenye furaha) waweza kusema They are happy. ( Hapa THEY , inawakilisha John na Juma ikimaanisha WAO).
Mifano mingine ya viwakilishi vya nafsi ni
HE, HIM – Yeye (Mwanaume)
SHE,HER,  - Yeye (Mwanamke)
IT,   - Yeye (Kitu)
THEY, THEM- (Wao)
WE, US,-(Sisi)
I , ME -(Mimi)
Baada ya kusoma maelezo ya aina za personal pronouns utaelewa kwa nini tuna maneno mawili tofauti ya personal pronouns kwa kila aina ya kiwakilishi hapo juu.

Aina za Personal Pronouns
Katika sentensi vitu au watu vinaweza kuwa mtenda au mtendewa. Tunasema mtenda wa tukio endapo mtu au kitu kinafanya tendo kwa kitu au mtu mwingine. Na huyo anayepokea tendo toka kwa mtendewa basi anakuwa mtendewa.
Mfano chukulia sentensi ifuatayo:
Juma anamfundisha Aisha.
Hapa Juma  anatenda (Mtendewa) na Aisha anatendewa (Mtendewa). Kama tukiandika kwa kutumia personal pronouns, tutapata sentensi hii.
Yeye (mwanaume) anamfundisha yeye(mwanamke)
He is teaching her.
Mfano huo hapo juu unatuleta katika aina mbili za personal pronouns, yaani subject personal pronouns, na object personal pronouns.  

Subject personal pronoun yaani  kiwakilishi cha nafsi mtenda, 
na 
Object personal pronoun ni kiwakilishi cha nafsi mtendewa.

Matumizi ya Personal Pronouns
Kuelewa vema aina hizi za viwakilishi kunakuwezesha kutunga sentensi zinazoeleweka na kukufanya uje uelewe vipengele vingine vya lugha kama kuandika Passive Voice, yaani sentensi ambazo zinalenga kuanza kumtaja mtendewa wa tukio kwanza.

Passive Voice ni somo pana na linahitaji uelewa mzuri wa aina za personal pronouns kama tulivyotaja hapo juu, na pia uelewa mpana wa aina za nyakati.

Kwa kua tumekwisha jifunza  aina za nyakati za wakati uliopo, ngoja nikudokezee walau mifano miwili ya Passive Voice uone matumizi ya Personal pronouns

Active Voice
He teaches her.— Yeye (mwanamme) anamfundisha (mwanamke).
Hapa mtenda ni yeye (mwanaume) na kwakua ni mtenda, tumetumia HE, mtendewa ni yeye (mwanamke) tungeweza kusema SHE, ila tukumbuke kuwa katika sentensi hii yeye mwanamke ni mtendewa hivyo basi inabid tutumie HER.

Passive Voice : 
Kumbuka passive voice huanza na mtendewa. Ambaye kwa sentensi yetu ni yeye(mwanamke).
Hivyo itakuwa:
She is taught by him. Yeye  (mwanamke) anamfundisha (mwanaume)
Hapa utaona kuwa hatujatumia HER, mwanzoni kwakua tunaanza na YEYE(mwanamke) kama mtenda na uliona hapo juu kuwa kama yeye mwanamke ni mtenda ni SHE na kama ni mtendewa inakua HER.
Kwa mwanaume tumetumia HIM badala ya HE, kwakua tuliona hapo juu kuwa HE ni kwa mtenda na HIM ni kwa mtendewa.

Hitimisho
Jitest 
1.You and ………….. (I, Me) are brothers. ( Wewe na Mimi ni mtu na kaka ake).    
      2. She has invited ………….(We,US). ( Yeye ametualika sisi)
      3. They were taught by.......... ( She, Her) Walifundishwa na yeye (mwanamke)
     4.………..(He,Him) always bring his daughter here. (Yeye mwanaume daima humleta mtoto wake hapa).
Nitumie majibu yako kwa WhatsApp +57 301 297 1724 au niachie ujumbe kwa ukurasa wetu wa Facebook, bofya hapa kuenda kwa ukurasa wetu.


Share:

0 comments:

Post a Comment