JE UNAANZAJE KUJIAMINI NA KUFANYA MAMBO MAKUBWA ?

Watu wengi wanaamini kuna watu maalum wa  kufanya  vitu fulani na tunaamin wanaofanya wana akili nyingi  au imepangwa iwe hivyo . Hata hivyo kwa kiwango kikubwa imani hiyo siyo kweli. 
Mfano kuongea kingereza kizuri mpaka usome shule nzuri au kufaulu lazima usome shule nzuri na hii ipo hata kwa wazazi huamua kuwapeleka watoto wao shule fulani wakitumaini moja kwa moja watoto wao watafaulu tuu. Ingawaje ni kweli shule nzuri inaweza saidia, ila bado ukweli unabaki pale pale kuwa zinahitajika   juhudi za ziada katika kufanikisha mafanikio kwa mwanafunzi.
Lengo la mfano wa imani kuhusu shule  ni kudokeza namna ambavyo tumekuwa na mazoea ya kutotazama na kutilia maanani uwezo wa mtu , pia kufuata mkumbo au kufanya mambo kwa mazoea.na wanafundisha vizuri lakini hajui kufaulu kunaanzia na juhudi za mtoto wake .

Mfano huu pia una lengo la kudokeza namna ambavyo mazingira yana changia sana  kutotimiza ndoto zetu na kusema hatuwezi.

Je ufanyaje ili uanze kujiamini ?
Kuamin unaweza haitoshi kufikisha malengo, ili kutimiza haya unapaswa  kuchukua hatua na kwa kuanza kutenda  ilo jambo kupangilia mda wako  vizuri,  kufanyia mazoezi na kujaribu mara kwa mara  bila kuchoka wala kukata tamaa.
Unahitaji kuelewa kuwa  mafanikio nikule kutimiza  ndoto zako kwa kufanya kile ambacho ulidhani hauwezi kufanya .mafanikio yanaweza  kuchukua muda, lakini kufanikiwa kunahitaji hatua kwa hatua kwa kua mafanikio ni safari.  

Hitimisho
Hivyo kumbuka wewe pia unaweza kufanya mambo makubwa sana. Unahitaji:
Kupagilia  mda 
Kufanya mazoezi
Kusoma vitabu na majarida  kupata ujuzi zaidi

Kuwa karibu   na kuomba   ushauri au msaada kwa wale wanajua au wenye uzoefu zaidi.
Share:

0 comments:

Post a Comment