MBINU ZA KUJIFUNZA ENGLISH KWA URAHISI -2

mbinu za kujifunza kiingereza kwa urahisi
Picha na footer.com

Huu ni muendelezo wa makala kuhusu mbinu za kujifunza lugha ya kiingereza. Tafadhali pitia pia sehemu ya kwanza ya makala hii. BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA KWANZA.
Lengo la makala hii ni kukupatia ufahamu wa kuwa kujifunza lugha ya kiingereza si tuu kujifunza kanuni za lugha hiyo na kuongea, ila unahitaji pia kuwa na mpangilio wa namna ya kujifunza ili uweze kujifunza kwa haraka na kwa urahisi.

6. Kufahamu miundo mbalimbali ya sentensi na kanuni za kufuata katika kila muundo:

Unapojifunza lugha unatakiwa kukumbuka kuwa kila unachoandika, kuongea, kusikia au kusoma ni SENTENSI.  Hata hivyo sentensi zimegawanywa katika makundi tofauti tofauti ili kukusaidia kujua kanuni sahihi kwa kila kundi la sentensi. Angalia hapa chini aina ya sentensi na  matumizi yake.
Kwa mtazamo wa lengo kuu ujumbe unaotolewa katika sentensi:

Sentensi ya maelezo chanya : Anaimba vizuri.  He is singing well.
Sentensi ya kukanusha. Haimbi vizuri. He is not singing well.
Sentensi ya kuuliza. Je anaimba vizuri ? Is he singing well ?
Sentensi za kutoa amri na sentensi za kuomba:  Sit down ! May I sit ?

Kwa mtazamo wa nani uhusiano kati ya mtendaji na anayetendewa
             Active Voice :
Mfano : He is writing a  letter Yeye anaandika barua.
Passive Voice  : Mfano a letter is being written by him. Barua inaandikwa na yeye.

7. Mbinu za kujifunza maneno mapya:

Ni wazi kuwa  kujifunza maneno mapya bila kuyakumbuka hakutokusaidia kuelewa hivyo wakati unakutana na neno jipya fanya jitihada ya kutafuta kitu cha kukumbusha  neno hilo jipya ulilojifunza. Fanya kulinganisha au kuhusanisha neno husika na neno fulani mfano kama neno PURE ni geni kwako, basi sema aah PURE nafahamu neno lingine linaloitwa hivyo ambalo ni KANDE ila kwa kipare. Hivyo unasema PURE (Halisi kwa kiingereza) inaweza pia kuwa KANDE kwa kipare.
Mbinu nyingine ni kuangalia namna ya kuongezea maneno mengine ya lugha husika yanayoendana na neno moja jipya ulilojifunza. Mfano kama kwako neno SHUT  (Kufunga) ni geni kwako, basi fikiria maneno mengine kama vile  OPEN (Fungua), au jiulize neno hilo linaweza kutumika na maneno mengine yapi mfano MLANGO (DOOR),  DIRISHA (WINDOW). Hivyo unakua umehusanisha kitendo cha kushut na vitu vinavyotumika na hicho .

Hitimisho:
Kwa ujumla wake makala hii imekuonyesha kuwa kujifunza English ni zaidi ya kusikiliza, na kusoma , unahitajika wewe mwenyewe kuingia hasa katika mchakato wa kuelimika kwa kufanya bidii kujikumbusha na kurahisha namnaya kuelewa unachosoma.
Pitia masomo ya KIINGEREZA katika ukurasa maalum wa KIINGEREZA. BOFYA HAPA

Kwa msaada wa maelekezo binafsi ya kufahamu vema lugha ya kiingereza. Wasiliana nami kwa WhatsApp +57 301 297 1724 au kwa John.myungire@gmail.com
Share:

0 comments:

Post a Comment