MAANA YA PROGRAMMING NA JINSI YA KUANZA KUANDIKA CODE

maana_ya_programming,anza kuprogram,andika code
Picha na foter.com
Ni ukweli usio na ubishi kuwa kwa sasa  programs, software au wengi tunazifahamu kwa jina la applications (Apps) ndio sehemu ya teknolojia inayoongoza karibu kila kitu katika maisha.  Iwe maisha yako binafsi, elimu, mahusiano, biashara, uzalishaji , afya , ulinzi na hata usafiri na burudani vyote vinahitaji programs.

Maana ya programming
Kwa kifupi programming ni shughuli ya kuandika programs, ambazo pia huitwa software au apps.
Yaani ni namna ya kuifundisha kompyuta ambayo ni mashine tuu, jinsi ya kutimiza hizo kazi unazotaka kufanikisha kupitia hiyo kompyuta.  Utaifundisha kompyuta kupitia maandishi maalum utakayoandika ambayo kompyuta zimetengenezwa kuyaelewa na hivyo kufanya hayo unayotaka ifanye.
Maandishi hayo maalum unayoandika ili kompyuta iweze kufanya kazi unazotaka ifanye , huitwa codes.
Codes huandikwa kwa kutumia lugha maalum ambazo zinatafsiriwa na kueleweka kwa kompyuta. Lugha hizo huitwa programming  languages.  Zipo programming languages nyingi sana kutegemeana na aina ya program unayotaka kutengeneza , mahitaji ya spidi, na wapi unataka program ifanye kazi. Majina ya baadhi ya program ni kama vile C, C++, Java, PHP, Python, JavaScript, Ruby na Scala.
Mfano mzuri wa program ni kama Facebook, ambapo wewe unaweza kuingia na kuandika ujumbe wako na kupost ili watu wauone.  Kuna mtu au watu walioandika hiyo program iitwayo Facebook inayokupa wewe nafasi ya kufanya unayotaka.

Faida za kujua programming
Hivyo basi kufahamu programming na kwanini watu wengi wanahitajika kujifunza programming tunatakiwa tufahamu kuwa programming  ni  namna ya kutengeneza zana (tools) ambazo watu wanaweza kutumia kufanikisha mambo kadhaa. 
Mfano ilivyo Facebook ni kwa ajili ya mawasiliano.
Kwa hiyo programming inaanzia kwenye kujenga wazo la matumizi ya kitu fulani utakachokiita program, mfano yaweza kuwa unataka kuwa na program ambayo itakufanya utunze kumbukumbu za matokeo ya watoto wako, picha za matukio ya familia, nk. Hayo ni mambo unayotaka kuyafanya kupitia program au app fulani.

Mfano rahisi wa kuandika program
Mfano  ili kama lengo lako ni program itakayowakaribisha wageni nyumbani kwako kwa kuwauliza majina yao kisha kusema karibu na kutaja jina la mgeni husika.
Hivi ndio muonekano wa program yako unavyoweza kuwa:
Mgeni anapewa nafasi ya kutaja jina lake kisha anabofya OK
Halafu mgeni anakaribishwa kwa kutumia neno Karibu kisha kutaja jina lake

 Program hiyo imeweza kuandikwa kwa kutumia code ifuatayo :
Programming language iliyotumika kuandika program hii inaitwa JavaScript


Programming itakufikisha wapi ?
Hivyo basi ukijifunza kuandika codes utaweza kuandika programs za kufanya mambo mengi unayotaka kuyaona yakitokea. Mfano programs nyingi zimeanzishwa kwa sababu programmers walitaka kutimiza mahitaji fulani kupitia programs ambazo hazikuwepo. Mfano Mark Zuckerberg wa Facebook anasema hivi kuhusu Facebook:
When I made Facebook  my goal was to help people understand what was going on in their world a little better. I wanted to create an environment where people could share whatever information they wanted, but also have control over whom they shared that information with.
Yaani kwa kifupi alitaka awe na program anayoita mazingira ya mtandaoni ambapo watu wanaweza kushare taarifa mbalimbali . Na hivyo ndivyo ilivyo Facebook mpaka leo.
Ili kutengeneza hicho alichotaka kukitengeneza ilimbidi aandike Codes, kama tulivyoona maana ya codes hapo juu. Na ilimbidi atumie programming languages. 
Na kwa kiwango kikubwa Facebook imeandikwa na inaendeshwa kwa kutumia programming language iitwayo PHP. Programming languages nyingine zinazotumika katika kukuletea Facebook unayoitumia pengine kila siku ni pamoja na Java,  Python, C++, Hack, Erlang, D, Haskell, na Xhp.

Hivi karibuni rafiki yangu wa Morogoro, Tanzania aitwaye Elias Tyrphone, akishirikiana na wenzake walitengeneza App kwa ajili ya watu kuitumia kutoa taarifa za watu waliopotea. App hiyo inaitwa NitafuteApp. Huu ni mfano wa jinsi programming inavyoweza kusaidia kutatua matatizo ambayo wewe unayaona katika jamii na yanahitaji program.

Hitimisho
Je umeelewa maana ya programming ? Ni matumaini yangu kuwa utahamasika nawe kuanza kujifunza kuandika codes ili uweze kuandika programs zitakazotatua hayo unayoyawaza iwe ni kwa ajili ya familia yako, masomoni, marafiki zako, biashara yako au hata kutengeneza programs/apps ambazo jamii kwa ujumla itazitumia.
Usikose sehemu ya pili ya makala hii ambapo tutaangalia namna ya kuanza kujifunza kuandika codes.

Ila waweza anza kujifunza codes kupitia websites hizi, au cheki vitabu vya lugha mbalimbali vya bure kwa kubofya hapa.
Share:

8 comments:

  1. Noted,Kupitia makala hii najua Wengi watatamani na wataweza maana makala ime pangiliwa kwa lugha rahisi sana inayoeleweka hata kwa asiyejua sana computer ana elewa.

    ReplyDelete
  2. asante,je ni wapi naweza kujifunza javascript

    ReplyDelete
  3. Nashukuru kwa msaada lakin nataka kujua zaidi programming c

    ReplyDelete
  4. Nimekuelewa lakn hzo code kila program inacode jinc ya kuziandika ama vp

    ReplyDelete