HUU NDIO USHAHIDI WA UTOFAUTI WA UBONGO WA MWANAMKE NA MWANAUME

Kuna ushahidi wa kisayansi kuwa ubongo wa mwanamke na mwanamme umeumbwa tofauti ndio mana :-
1. Kuna aina fulani ya shughuli au matukio mwanamke anaweza kufanya kwa ubora zaidi kuliko mwanaume, na kuna nyingine mwanaume anaweza kuwa bora zaidi kuliko mwanamke. 
Mfano, shughuli zinazotumia nguvu/misuli mwanaume anaweza kufanya kwa ubora zaidi kuliko mwanamke, wakati shughuli zinazohitaji kumbukumbu na kujenga picha ya mbali -bila kuwa na taarifa (intuition) basi wanawake ni bora zaidi. 
Mfano mwanamke ni bora zaidi katika MALEZI YA MTOTO kwa sababu ya uwezo wake wa kugundua mambo hata kama hakuwepo, na uwezo wake wa "kutabiri" yajayo hata kama hana taarifa rasmi kuhusu hapo baadae. 
 
2. Wanawake wana uwezo wa kubeba mambo mengi vichwani mwao na kukumbuka vitu vingi kuliko mwanaume ambaye huwa na jambo moja au vitu vichache tuu anavyoweza kufanya kwa wakati mmoja. Wanawake ni wazuri katika "multi-tasking"-yaani kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja.

---Ushahidi wa kisayansi kuhusu utofauti wa ubongo wa mwanamke na mwanaume, unaelezwa na watafiti toka chuo kikuu cha Pennsylvania cha huko Marekani kama walivyonukuliwa na jarida la mtandaoni la MEDICALNEWSTODAY.COM.
Picha na Medicalnewstoday

--Utofauti wenyewe wa ubongo ni muundo wa jinsi "nyaya" za ubongo zilivyounganishwa. Wanawake wao nyaya zao zimeunganishwa toka upande mmoja (kushoto/kulia) kwenda upande mwingine, wakati wanaume wao ubongo "nyaya " zake zimeunganishwa toka mbele kwenda nyuma na kwamba "waya" mmoja hauwezi kuwa pande mbili za ubongo, yaani kama waya upo upande wa kushoto basi utapita toka mbele kwenda nyuma upande huo huo wa kushoto. Hivyo hakuna mawasiliano upande mwingine wa kulia.
Share:

0 comments:

Post a Comment