UMEWAHI KUSIKIA HABARI YA CHURA NA MAISHA YETU ?

Tafakari yetu leo  inahusu hadithi maarufu ya CHURA.
Mwanasayansi toka ujerumani Heinzmann, aligundua kuwa chura akiwekwa kwenye chombo tuseme sufuria  yenye maji baridi , halafu maji hayo yakaanza kupashwa moto kidogo kidogo , basi chura huyo wala hatohangaika kutoka kwenye maji, na hatimaye kufa wakati maji hayo yatakapokuwa ya moto kweli kweli. Ingawaje kuna mabishano ya kisayansi kuhusu usahihi wa madai ya Heinzmann, leo utajifunza kitu kuhusu habari hii ya chura.

Kumbuka ukimweka chura kwenye maji ambayo tayari ni ya moto , atakurupuka haraka. Utafiti nilioleza hapo juu ni kama utamweka kwa maji ya baridi.
Mara nyingi ili binadamu akubaliane kwa urahisi na mabadiliko, basi mabadiliko hayo ni lazima yafanyike kidogo kidogo kama hiyo habari ya chura.

Jamii yetu inaporomoka kimaadili siku hadi siku, kiwango cha elimu kinashuka na hata ufanisi makazini ni ishu. Hata hivyo matatizo hayo ya mfumo wetu wa maisha hayajaanza leo,  hayakuwa makubwa kiasi hiki kipindi kirefu kilichopita,  ila yameendelea kukua kidogo kidogo kama vile yale maji yanavyoongezwa joto ili kumuunguza chura. Hatukusikii wala hatuoni ni shida, tumebaki kulaumiana ila mbaya zaidi kama vile yule chura, bado hatuchui hatua ya kujikwamua kwa haraka kwa kuwa ni kama tumekwishajizoelea hali hii.


Bado unayo nafasi ya kuamka, na kubadili kile kinachokukera. Usikatishwe tamaa na mfumo mzima wa maisha ya jamii, mabadiliko ya kweli ya jamii hayategemei wote sisi kubadilika kwa wakati mmoja. Kila mmoja wetu akibadilika kidogo kidogo jamii itafika mbali.
Share:

0 comments:

Post a Comment