STORI ISIYOELEZWA NA WENGI KUHUSU DIDIER DROGBA..

Picha na moonofthesouth.com
Katika mahojiano yake  na kituo cha runinga cha ITV, yaliyorushwa hewani tarehe 10/12/2013  Didier Drogba alizungumzia hivi kuhusu kuhamia kwake Uingereza toka timu iliyompatia umaarufu nchini Ufaransa ya Olympique Marseille

“Yeah there was some moments when I was saying maybe it’s not for me. Maybe I go back to France, I go back to Marseille because I still had that feeling for Marseille but then I’m you know, I’m a fighter and I was like, ‘No, I came here and I need to achieve something, I need to achieve something and I need to make history here.’ 

Yaani :
Kuna nyakati nilikuwa nasema kuwa pengine hii sio kwa ajili yangu. Labda tuu nirudi Ufaransa, nirudi Marseille kwa sababu bado nilikuwa naipenda Marseille, ila wajua, mie ni mpiganaji, na nikawa kama, Hapana nilikuja hapa na ninahitaji kufikia kitu fulani.  Nahitaji kufikia kitu fulani, na ninahitaji kuweka historia hapa".

Na Drogba anaeleza hivi kuhusu namna anavyojisikia hususani akirudi kwao Ivory Coast:

“First of all I don’t see myself as a superstar, I see myself as a normal guy, one of these guys who had more chances, who was lucky to have his parents behind him to give him the chance to have a good chance in life. So when I go there I don’t know, I always feel that I was lucky to have met that journey because a lot of them some people are better than me, some of the guys there that are playing are much better than me but they didn’t have the chance I had so I do not see myself as a superstar.”
Yaani: 
" Kwanza kabisa, sijioni kama ni superstar. Najiona kama mtu wa kawaida tuu, mmoja wa hawa (wa Ivory Coast) ambaye alipata nafasi zaidi , mtu ambaye alikuwa mwenye bahati ya kupata wazazi wa kumpa nafasi ya kuwa na nafasi nzuri kimaisha. Hivyo ninapoenda kule (Ivory Coast) , daima hujisikia kuwa ni mtu mwenye bahati ya kukutana na ile safari (ya mafanikio) kwa kuwa wapo wengi kati ya hawa watu (wa Ivory Coast) ambao wanacheza vizuri zaidi yangu, ila hawajapata nafasi kama niliyoipata mie, hivyo sijisikii kama ni superstar".

Embu soma kwa uchache wasifu wa Didier hapa chini:-(kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vilivyonukuliwa na Wikipedia.)
  1. Jina lake kamili ni Didier Yves Drogba Tébily
  2. Didier hakuwahi kucheza katika Soccer Academy yoyote
  3. Alianza mpira wa kulipwa akiwa na miaka 21
  4. Timu yake iliyomtoa - Levallois Sporting Club ya Ufaransa imeupa jina uwanja wake jina la Didier Drogba
  5. Drogba alichangia kutoka mfukoni mwake paundi Milioni 3 alizopata kwa tangazo la Pepsi kwa kujenga hospitali huko nchini kwao Ivory Coast.
  6. Drogba ana asasi yake isiyo ya kiserikali iitwayo  "Didier Drogba Foundation" na katika kumuunga mkono, Chelsea imechangia fedha za kuendesha asasi hiyo. Drogba ndiye Raisi wa asasi hiyo.
  7. May 9,2011 Drogba alisusia kushangilia goli wakati wachezaji wenzake wote walikuwa wakishangilia goli lililofungwa na Frank Lampard kwa njia ya penati.. Kisa ? Eti alitaka apewe yeye afunge ili awe mfungaji bora wa ligi kwani alikuwa amebakiza goli moja tuu kumzidi Wayne Rooney. Hata hivyo katika mechi hiyo ya Chelsea na Wigan Athletic, timu yake ikapata nafasi ya penalti na hapo akaachiwa nafasi naye akashinda na kuwa mfungaji bora wa msimu wa 2010-2011.
  8. Mbali na soka, Didier Drogba ana elimu ya uhasibu.
  9. Drogba ndiye mchezaji aliyefunga magoli mengi zaidi katika historia ya timu ya Taifa ya Ivory Coast.
  10. Drogba pia ndiye mchezaji wa kigeni (mchezaji toka nje ya Uingereza) mwenye magoli mengi zaidi ya kufunga kuliko wachezaji wote wa kigeni.
  11. Drogba alianza kuvaa namba 15 alipohamia Chelsea, hadi pale Damien Duff alipohama Chelsea ndipo akachukua namba 11 aliyokuwa akiitumia Duff. 


Share:

0 comments:

Post a Comment