HAYA NDIO UNAYOKOSA KWA KUTOKUSHUKURU KWA UFASAHA..

Yawezekana ikaonekana kama ni jambo dogo sana kushukuru lakini shukrani ya kweli kwa mtu mzima kama wewe sio tuu kusema ahsante, bali shukrani ina maana ya kuwa:-
1. Umethamini ulichopewa
2. Umeiona hisani au huduma ya mtu husika
3. Unatambua kuwa ni jambo jema limekutokea kwamba mtu fulani kakupatia kitu au huduma fulani. Ni kama vile kujinyenyekeza kimoyo moyo na kujiambia kuwa pengine wala haukustahili kufanyiwa hivyo ulivyofanyiwa, au kupatiwa hivyo ulivyopatiwa bali ni kwakuwa imekuwa jambo la kheri kwako kupata ulichopata.

Maana hiyo ya shukrani sio tuu kwamba kwa wale wanaokusaidia au kukupatia vitu BUREE, bali hata kama unalipia , bado unahitaji kushukuru kwani wapo wengi wanaolipia huduma au bidhaa na bado wasipate huduma nzuri au wasipatiwe kile wanachohitaji.

Swala la ahsante sio tuu kwenye biashara. Ahsante ni swala la msingi hata katika mahusiano -mume inabidi amuambie ahsante mke, na mke kwa mume pia kwa sababu hizo hizo.
Watoto kwa wazazi pia.Wanafunzi kwa walimu n.k


Hata kama ni mzazi, mwalimu au mpenzi amekutendea jambo jema, usijione kuwa ni eti ulikuwa na haki ya kutendewa hivyo ulivyotendewa hivyo basi hauna haja ya kushukuru.

Kushukuru kwako kwa ufasaha bila kusanifu, kunamgusa mtu husika hivyo kuna muandaa au kumpa hamasa ya kukutendea jambo jema lingine. Ndio maana wanasema KUSHUKURU NI NAMNA NYINGINE YA KUOMBA.

Utaona kuwa shukrani sahihi inakufanya uthamini ubinadamu, shukrani sahihi inakufanya ujitambue vema na kukumbusha kuwa una thamani kwani mtu mwingine amekujali kufanyia hicho ambacho unasema ahsante.
--Mara baada ya kusema hivyo, napenda niseme ahsante kwako msomaji wa Mbuke Times. Uwepo wako na support yako inanipa nguvu ya kutafakari mambo kila siku. Mie pia ninanufaika.



Share:

0 comments:

Post a Comment