JE CHUMBA CHAKO CHA KULALA NI KAMA STOO ? SOMA HAPA..

Je, chumba chako ni kama stoo? Umejaza vitu chini ya uvungu wa kitanda? Je mara nyingi umejikuta unatafuta hata vitu vidogo tuu ambavyo pengine ulidhani unajua wapi vilipo? Basi makala hii inakuhusu.
Fikiria umeenda ofisini kwa mtu, una haraka zako ila unahitaji mtu huyo atie saini nyaraka yako ambayo uliiwasilisha hapo wiki moja iliyopita. Kufika hapo anachukua dakika 20 kutafuta wapi nyaraka ipo (kwakuwa vitu vyake vimejipanga hovyo). Unamuona wakati anatafuta nyaraka yako, anaochana nyaraka nyingi ambazo zinaonekana hazina umuhimu tena kwa ofisi yake ila zilikuwepo tuu hapo ofisini.Baada ya kuipata hiyo nyaraka anagundua kuwa hana kalamu.
Baada ya kuhangaika kuitafuta kalamu hapo ofisini kwake, amekata tamaa anaamua kuenda ofisi ya jirani kuazima. Hata hivyo huko nako anacheleweshwa kwakuwa huyo aliyemfuata naye haioni kalamu kwa urahisi.
Ndivyo pengine hata wewe ulivyo, una vitu vingi usivyovihitaji ila umevirundika bila sababu ya msingi. Ok, sababu yako kuu ya msingi yaweza kuwa unatumaini kuvitumia hapo baadae. Lakini kwa kuwa hauna taratibu ya kupitia vitu vyako basi unajikuta umeweka vitu vingi bila msingi.
Na waweza dhani kuwa hakuna tatizo katika kutunza vitu hivyo usivyovihitaji ila embu kumbuka jinsi vinavyojaza chumba chako, aun yumba yako. Kuna watu vyumba vyao vya kulala ni kama “stoo”, embu chunguza chini ya kitanda hivyo ulivyojaza unavihitaji kweli , embu chunguza juu ya meza yako iwe ya ofisini au nyumbani unahitaji , embu chunguza kabatini na kwenye mabegi yako, jee hivyo vitu vyote pamoja na nguo kweli unazihitaji.
Tatizo la kujaza vitu vingi visivyo  na umuhimu kwako ni KUPUNGUZA UFANISI wako kwakuwa utajikuta muda mwingi unatumia kutafuta vitu vya umuhimu kwa kuwa vimesongwa na hivyo visivyo vya umuhimu.

Kupunguza vitu visivyo na umuhimu haitoshi, jitahidi pia kupangilia vema vitu vyako. Kumbuka kwanini mara nyingi unajisaidia haja kubwa au ndogo ? ni kwa sababu hata mwili wako unahitaji kuondoa yale yasiyohitajika mwilini, ili uendelee kuwa mwenye afya. Ndivyo na wewe unahitaji kupunguza hayo yanayokuzunguka ili uwe mfanisi zaidi.
Share:

0 comments:

Post a Comment