HIVI NDIVYO VITU VINAVYOJIPOST KWA AKAUNTI YAKO YA FB BILA WEWE KUJUA

Ndiyo mara nyingi watu wamekuwa wakilalamika kuwa kuna watu wanapost vitu kwa akaunti zao za FB bila ruhusa. 

La msingi kuelewa ni kuwa kwa kiwango kikubwa chanzo cha hao watu kupost kwa akaunti yako kama vile ni wewe ndiye unayepost, ni kwakuwa wewe mwenyewe umeruhusu kufanya hivyo.

Haijalishi kama umetoa ruhusa kwa kukusudia au kutokukusudia , lakini ni wewe mwenye akaunti ya FB ndio chanzo cha matatizo hayo.
Kivipi ? 

1. Unapo comment kwa websites au blog
Mfano wa sehemu ya kuacha comment. Picha na Techcrunch.com
Kuna websites na blogs nyingi hutumia kitu kiitwa Facebook plugin, yaani mkusanyiko wa codes fulani ambazo pamoja na kuruhusu kupost katika website au blog husika, pia huonyesha ulicho comment kwa akaunti yako ya Facebook.

2. Unaporuhusu apps kutumia akaunti yako
Kuna namna mbili za kuruhusu apps kutumia  akaunti yako:
A. Kwanza: Ni wewe mwenyewe unakuwa unajua kabisa kuwa unaruhusu app husika kufanya hivyo. Mfano kama umetembelea website ya yahoo au bbc na ukakubali kujiandikisha kwa application (app) yao, basi utapata maelekezo kuwa unatakiwa uruhusu app husika itumie taarifa za akaunti yako, na pia itakueleza kuwa kuna wakati inaweza ikapost vitu kwa niaba yako.
Hivyo kama hautaki app ifanye hivyo hakikisha unaacha kukubali hayo maelezo. Hivyo hautoweza kuitumia hiyo app.
Usiposoma makini vitu kama hivi waweza kukuta unaambiwa kabisa kuwa app itakuwa ikipost kwa niaba yako, ila wewe unakubali tuu.
B. Pili: Waweza kuruhusu app bila wewe mwenyewe kujijua. 
Hii inaweza kutokea pale ambapo una click tuu link usiyoijua na kujikuta unapokea maelekezo tofauti tofauti. Maelekezo mengine yanaweza kukuchanganya na kwakuwa waweza kuwa na haraka ukajikuta usisome kwa umakini maelekezo unayopokea hivyo kubofya sehemu ambayo itapelekea kutoa ruhusa kwa apps kuitumia akaunti yako. Angalia mfano pichani mwanzoni kabisa ambapo post inakudanganya kuhusu mwanamieleka wa WWE na wewe kwakuwa unataka kufuatilia habari utabofya link. Kubofya kwa link kama hizo kwaweza kukupelekea kuruhusu watu wengine watumie akaunti yako.

3. Unapokuwa umeibiwa akaunti yako bila kujijua
Kuna namna mbalimbali za kuibiwa akaunti yako ya FB bila kujijua:-

A. Kwa ku-sign in akaunti yako ya FB katika website feki ya FB:  Kuna watu wanaweza kutengeneza websites zinazoonekana sawa sawa kabisa na FB hata hivyo kiukweli sio, katika lugha ya kitaalamu mtindo huu unaitwa phishing.  Hivyo wakishakuingiza mjini na kupata password na jina lako unalotumia FB, wanaweza kuitumia akaunti yako kwa namna yoyote wanayopenda wao.

Kwa kuruhusu extension maalum zinazohusu Facebook: Fahamu maana ya neno extension ni kuwa ni program maalum unayoingiza katika kompyuta yako ili kusaidia web browser kama Mozila Firefox, Internet Explorer au Google Chrome ili kuboresha ufanyaji kazi wa browser husika au kukupa uwanja mpana Zaidi wa matumizi ya website fulani utakayoitembelea. Mfano zipo Facebook extension iitwayo Facebook Chart Alert inakuwezesha kupata notification kuwa rafiki yako ame sign in FB pale mmoja wa rafiki yako afanyavyo hivyo. OK, natumaini umeelewa maana ya EXTENSION.

Hitimisho : Je, dawa ni nini ?
Elewa kuwa una jukumu la kuwa makini wewe mwenyewe ili usikumbwe na majanga hayo hapo juu. Mfano hakikisha hau click links usizozijua. Hakikisha unasoma maelekezo vema ya chochote kinachojitokeza wakati unatumia FB kujua kama kinakutaka ukiruhusu kitumie akaunti yako.
Pia hakikisha unakuwa makini na website ya Facebook unayofungua kwani pengine ni feki. Hata unapodownload apps kwa ajili ya matumizi ya FB kama vile Facebook Messenger hakikisha umeitoa sehemu kweli ya kuaminika kama vile Google Store.

Kuhusu kuondoa APPS usizozihitaji
Ingia kwa settings za akaunti yako sehemu ya APPS (Cheki kushoto kwa kompyuta yako) kisha fuata maelekezo katika ukurasa huo wa APP kwa ku remove app husika.

Share:

0 comments:

Post a Comment