TWITTER: NINI NA NAMNA UNAVYOWEZA KUITUMIA

Kama unataka kuwa “up to date” na taarifa mbalimbali ziwe ni makala toka website mbalimbali au habari za matukio mbalimbali, basi twitter, ndio njia maarufu sana katika kukufanikisha katika hilo. Makala hii inakupa maelezo ya jinsi ya kuanza kuitumia twitter, na pia kama umeanza kutumia basi inakupa mwanga zaidi wa mambo ya msingi kufahamu ili kuboresha matumizi ya twitter.

Twitter ni nini

Twitter ni mtandao unaokuwezesha kuandika ujumbe mfupi wa maneno usiozidi maneno 140 na ku ‘share’ . Ujumbe huo wa maneno 140, ndio huitwa ‘tweet’,  na kitendo cha kuandika na kurusha hewani ‘tweet’ yako ndio huitwa “ku tweet”.
Unaweza pia ‘kushare’ tweets za watu wengine, kitendo cha kushare tweets za watu wengine huitwa “ku retweet”.
Unaweza pia kutuma ujumbe kwa mtu binafsi aliyejiunga na tweeter, endapo umejiunga nae katika mawasiliano yenu ya tweeter.

Je unajiunga vipi na twitter
Ili kujiunga na twitter, kwanza inakupasa uwe na anuani ya barua pepe (email address), kisha ingia www.twitter.com  na utaona sehemu ya kujisajili (sign up). Katika kujisajili kwanza utatakiwa kuandika Jina lako, na pia utatakiwa kuandika barua pepe yako, na uandike password utakayokuwa ukiitumia kufungua hiyo akaunti yako ya twitter. Ukishamaliza kufanya hivyo, bofya Sign Up for twitter, na utakutana na ukurusa mwingine ambapo utakuwezesha kuchagua aina la jina utakalotumia katika Twitter. Angalia sehemu imeandikwa “Choose your user name”.
Jina lako la twitter huitwa “handle”, hivyo mtu anaweza kuambia “Niambie twitter handle yako”

Je unapata vipi watu wa kuwasiliana nao kwa twitter
Marafiki waliokualika au kukujumisha wewe kama rafiki yao  katika twitter wanaitwa “followers”, na wale unaowajumuisha wewe wanaitwa “following”. Mara kwa mara utapokea kutoka twitter wenyewe mapendekezo ya akina nani uwajumuishe kama “following” wako, hata hivyo, wewe mwenyewe pia unaweza kutafuta kwa sehemu ya search katika twitter majina ya watu au habari unazotaka kufuatilia, kisha ukawajumuisha watu kama “following” wako kwa kubofya sehemu ya “follow”

Je unapost vipi ‘status’:
Kushoto mwa ukurasa wako wa twitter kuna sehemu imeandikwa “ Compose new tweet”. Hapo ndipo unapoandika status yako na kisha kubofya “ TWEET”. Utaona pia alama ya picha, basi bofya hapo kama unataka kupost picha.

Matumizi ya alama ya #
Kwa usahihi, alama ya # hutumika kuifanya status iingie katika kundi maalum la aina ya status. Mfano kama utaweka #Majanga, basi unailazimisha status yako iingizwe katika kundi la status zinazotumia hiyo alama ya Majanga. Hii ina maana kuwa kama kuna watu wengine wametumia hiyo alama ya #Majanga, basi nyote status zenu zitaorodheshwa huko.

Picha ya Profile yako
Kama ilivyo katika Facebook, unaweza pia kuweka picha mbili kwa profile yako, ili kufanya hivyo nenda sehemu ya kuedit profile yako, ( Kulia juu mwa akaunti yako kisha bofya edit profile). Utakuta sehemu ya kuweka Photo, na sehemu ya kuweka picha ya Header.

Kuunganisha akaunti yako ya twitter na Facebook
Ndio, unaweza kuamuru twitter iwe inaonyesha tweets zako kwenye akaunti yako ya Facebook. Ili kufanikiwa katika hilo, unatakiwa kuingia sehemu ya Edit Profile, kisha angalia sehemu imeandikwa Connect to Facebook. Bofya hapo kisha ufuate maelekezo utakayoambiwa.

Twitter katika simu yako
Ndio unaweza kuitumia twitter kwa urahisi ukiwa ume download na ku install program maalum kwa simu za mkononi. Ukiwa kwa simu yako, nenda google.com, kisha waweza andika Download twitter for (android) kama simu yako inatumia system za android. Kama ni Nokia, basi andika Download twitter for Nokia. Kisha chagua chaguo la kwanza linalokupeleka kwenye ukurasa wa kudownload hiyo program, ukiisha install, utaweza tumia vema twitter katika simu yako.
Hata hivyo, hata kama hauna program ya twitter, unaweza tumia twitter, kwa kuandika anuani ya twitter kwenye sehemu ya kuandika anuani za website yaani www.twitter.com, kisha fuata maelekezo kama unataka ku sign in, au ku sign up.
Share:

2 comments:

  1. Me Twitter yangu nikitaka kuingia inaniambia ,,I'm robot??nashindwa kuelewa why msaada pleas

    ReplyDelete