ZITAMBUE NAFASI ZA KAZI 'FEKI' ZA ONLINE

Umekua ukitamani kupata nafasi ya kufanya kazi, na kwa bahati nzuri siku isiyo na jina unapofungua inbox ya email account yako  unakutana na habari ya nafasi ya kazi , ambayo kiukweli inavutia kama barua pepe hii hapa:

“MARRIOTT HOTEL CANADA HAS EMPLOYMENT OPPORTUNITIES FOR AN EXOTIC
CANDIDATES IN DIFFERENT SKILLS,SEND YOUR CURRENT CV/RESUME AND APPLICATION
LETTER IN MICRO SOFT. (marriothotel_cn@hotmail.com)”

Bila shaka jambo la kwanza utakalofanya ni kutafuta wapi CV yako ipo, kisha fasta unatuma hiyo CV, ukisubiria wakujibu kwa kukueleza pengine aina ya kazi unayoweza kuapply.
Jambo la msingi unapopata email kama hiyo sio kuharakisha kuijibu. Email zozote zenye kueleza ‘ofa’ fulani ni vizuri kufanya uhakiki kabla ya kuzijibu. Kuna nafasi za kazi feki kama hizo hapo, na zaidi sana kuna matapeli wengine wa kwenye mtandao humu wanaoweza kukuingiza mjini kwa jinsi mbalimbali iwe kwa dili la kupata schorlaship, vyuo, misaada ya fedha n.k.
Email nyingine za nafasi za kazi feki zinaweza kuwa na maneno kama:

"After registering your Direct Deposit confirmation, please respond back to this email with your ideal interview date/time. Remember, you need your Direct Deposit account info prior to your interview, as we will be processing your payment information at that time."

Mbaya zaidi ni kuwa, kuna wakati unaweza kweli kutuma CV, yako ukajibiwa ujaze fomu ambayo inapatikana katika website fulani. Hapo kuna mawili, moja ukajikuta ukiwa kwenye hiyo website yako ya kujaza fomu, ukahamishwa na kupeleka kwenye website nyingine itakayokuwa feki. 

Au pili ukafanikiwa kweli kujaza fomu na hata ukapata kazi, ambayo ni kazi ya kufanya kwa mtandao. Baada ya wiki moja au mbili au hata mwezi kampuni hiyo unayofanya kazi ikakuambia imekutumia hundi. Na kweli ukapata details zote za hiyo hundi. Ila baada ya muda wakasema wamefanya makosa, katika kiasi fulani, hivyo inabidi urudishe kwa kumtumia mtu mwingine ambaye walikuwa wamemlenga. 

Hata hivyo ukweli ni kuwa hizo hundi walizokutumia ni feki, na kwamba utakapotuma fedha zako binafsi, ukiwa unasubiri kwa hamu kupokea mshiko wako, utajikuta unaambiwa na benki yako cheki ni feki.
Jihadhari, kumbuka msemo wa kiingereza usemao “ If a deal is too good to be true, think twice”. Usione haya kushurikisha wengine, ukiona email kama hizo. Uchoyo wa kuwaambia watu vitu unavyohisi ‘dili’ unaweza kukuponza.

Utazitambua nafasi za kazi feki kwa mambo kadhaa kama yafuatavyo:

  • Zinahitaji wewe kutanguliza malipo fulani

  • Zinahitaji maelezo yako binafsi ya kifedha- mfano namba ya akaunti yako ya benki

  • Ukitafuta kwa kutumia Google mfano, hauoni website ya kampuni husika inayotoa ajira

Share:

1 comment:

  1. Kweli kabisa hawa jamaaa wa Marriott Hotel Canada, hata mimi walinisumbua saana lakini mwiaho nikashtuka kuwa si wakweli,pilipia tanzania siku hizi katika mitandao ya kazi pia wapo matapeli, na kudai uwatumie kiasi cha pesa kwenye simu zao ili wakutumie maswali, uongo mtupu

    ReplyDelete