KWANINI INASEMWA PAPA MPYA ANAMILIKI TIMU YA SOKA?

Jina la timu ni San Lorenzo de Almagro, maskani yake ni Buenos Aires, huko Argentina. Timu hiyo inapatikana kwa website ifuatayo www.sanlorenzo.com.ar . Kisa cha watu kusema timu hii inamilikiwa na papa mpya, Papa Francis, ambaye jina lake halisi ni  Jorge Mario Bergoglio, ni kutokana na ukweli kuwa Papa Francis, ni mmoja wa wajumbe wa umoja unaomiliki timu hiyo, na yeye mwenyewe ana kadi ya uanachama wa timu hiyo.

Zaidi sana, hivi karibuni baada ya Papa huyo mpya kutangazwa, timu hiyo kongwe iliyoanzishwa rasmi kama klabu mwaka 1908, ilianza kutumia jezi maalum zenye picha za Papa huyo.
San Lorenzo de Almagro, pamoja na kushinda mataji 10 makubwa katika ligi daraja la kwanza huko  Argentina, haijawahi kushinda mashindano makubwa ya kimataifa,achilia mbali mashindano ya bara la America ya kusini. Ndio maana Lucas Roldan, mshabiki wa timu pinzani ya Boca Juniors amenukuliwa na nesn.com akiibeza San Lorenzo kuwa , kuchaguliwa kwa Papa huyo , ndio ushindi wa kipekee wa kimataifa wa timu ya San Lorenzo.

Timu ya San Lorenzo de Almargo, inahusishwa na kanisa katoliki kwakuwa hapo mwanzo vijana walikuwa wakicheza mitaani, lakini padri Lorenzo Massa, aliwaonea huruma vijana wa mitaani hivyo akawaita wacheze kwenye uwanja wa kanisa, na inasemwa kuwa yeye mwenyewe padri Lorenzo, ambaye baadae alikuja kutangazwa kuwa Mtakatifu, aliwahi kununua magoli ya uwanja huo, na alikuwa akiwafundisha dini wachezaji hao.

Habari hii ni kwa uchambuzi  toka:
www.nesn.com
Share:

0 comments:

Post a Comment