HISIA KALI ZA MAFANIKIO YA CRISTIANO RONALDO

Story ya mafanikio ya Cristiano Ronaldo iliyosambazwa katika mitandao mbalimbali imekuwa gumzo kwa jinsi ambavyo inagusa hisia za watu wengi. Baada ya kusoma makala hii, jiulize jee unaamini kama kweli Ronaldo mwenyewe alisema maneno haya, na kama alisema nini unajifunza. Ifuatayo ni tafsiri ya maneno yanayodaiwa kuwa Ronaldo ametaja kuwa ni siri kubwa ya mafanikio yake ya kujulikana katika soka:
“Inabidi nimshukuru rafiki yangu wa zamani, Albert Fantrau kwa mafanikio yangu. Tulicheza pamoja katika timu moja katika mashindano ya U-18. Wakati kocha wa Sporting Lisbon alipokuja kuitembelea timu yetu alisema “ Yoyote anayefunga magoli mengi katika mechi atapata nafasi ya kuingia katika academy yetu”
"Katika mechi tuliyocheza, timu yetu ilifunga magoli 3 -0. Mie nilianza kufunga goli la kwanza, Albert akaja kufunga goli la pili, na goli la tatu lilikuwa muhimu sana kwetu.
Albert alikuwa ameshawatoka mabeki na golikipa, nami nilikuwa nyuma yake. Alichotakiwa kufanya yeye ni kufunga tuu, ila alinipatia pasi mie, nikafunga, nikapata nafasi ya kuenda Sporting Lisbon Academy.
Baada ya mechi nikamuuliza kwanini alifanya vile, na akanijibu kuwa “ Wewe ni mchezaji bora zaidi kuliko mie”

Na hata waandishi wa habari walipomhoji Albert nyumbani kwake, Albert alikubali kuwa CR7 alisema kweli. Na Albert akaongeza kuwa siku hiyo aliyomuachia CR7 afunge goli, ndio siku aliyoiacha fani ya soka na akabaki hana ajira mpaka leo.

Waandishi wakataka kujua imekuaje sasa anamiliki nyumba ya kifahari na gari bomba tuu. Na anaonekana kuwa mtu tajiri. Mali zote anapata toka wapi ?. Albert akajibu “Vyote hivi vinatoka kwa Ronaldo”.


N:B
Habari hiyo hapo juu haina uthibitisho wa moja kwa moja toka Cristiano Ronaldo mwenyewe. Website nyingi zinazoandika maelezo hayo, hazielezi wazi Ronaldo alisema lini maneno hayo, ingawaje ni kweli kuwa Ronaldo ana rafiki ambaye kwa sasa hana ajira naitwa Albert Fantrau.
Share:

0 comments:

Post a Comment