MAUJANJA YA MSINGI KATIKA MICROSOFT WORD 2010

Inawezekana unaandika taarifa ndefu yenye kuhitaji uweke  namba za kurasa tofauti ili kuleta mvuto na uelewa fasaha wa taarifa husika. Mfano ungependa kurasa zinazoonyesha Yaliyomo (Table of contents) , Shukrani (Acknowledgement), Orodha ya vifupisho ( List of abbreviations) , na Ufupisho wa taarifa (Abstract), n.k  ziwe na namba za kirumi (I, ii, iii,n.k), halafu sura (chapters) za taaarifa yako ziwe katika namba za kiarabu/namba za kawaida yaani 1, 2, 3, …nk.

Makala hii inaangalia jinsi ya kuweka page numbers za kirumi na pia za kawaida, mfano ukurasa wa kwanza mpaka wa tano ziwe (i) –(v), halafu kurasa zinafuata namba zianzie 1, 2, 3,……n.k.

Tuchukulie mfano unataka kuwa na page numbers za kirumi kwa ukurasa wa kwanza mpaka wa tano, unachotakiwa kufanya nenda hadi ukurasa wako wa tano,  chini ya huo ukurasa wa tano, weka cursor mwisho kabisa wa maneno yote, kisha ingia PAGE  LAYOUT, halafu chagua, Breaks, halafu bofya sehemu ya  Section Breaks iliyoandikwa Next Page.

Baada ya kubofya hiyo section break ya Next Page ,  nenda moja kwa moja kwenye Insert, kisha Page Numbers, na kuchagua chaguo la Bottom ili namba zako zikae chini ya kurasa. Kisha bofya style unayotaka number iwe, bila shaka unataka namba ikae katikati.

Ukishapata page number iliyokaa kati, sasa unahitaji kufanya mabadiliko kidogo ya hiyo namba ili iwe ya kirumi. Kufanya mabadiliko  nenda  sehemu ya Format Page numbers kama unavyoona katika picha. 

Unaweza kuipata sehemu ya  Format Page numbers kwa kubofya pia INSERT kisha PAGE NUMBERS, halafu angalia katika menu zinazotelemka, utaiona hiyo Format Page Numbers.
Ukiwa katika Format Page Numbers ,  angalia menu  Number format, kisha chagua namba za kirumi, na kubofya OK.

Hapo tayari umeweka namba zako za kirumi toka ukurasa wa kwanza mpaka wa tano. Ili kuendelea na mtindo mwingine wa namba yaani 1, 2, 3, ….. kwa ukurasa unaofuata yaani ukurasa wa SITA, na kuendelea, nenda ukurasa wa sita, au wowote ule baada ya huo wa tano, kisha bofya INSERT, halafu PAGE NUMBERS, kisha fanya uchaguzi kadri utakavyo kama namba hizo zikae juu au chini, na kama zikae pembeni kulia, au katikati. Ukishafanya uchaguzi, bofya OK, na hapo tayari kazi yako imeisha.
Share:

3 comments:

  1. Aiseeee, ni somo la msingi sana, maaana wanafunzi chuo kikuuu huwa tunaadhirika sana

    ReplyDelete