INTERNET KUWA KWA KILA KITU, KILA MAHALI

Ndio, wanasayansi na wataalamu wa mambo ya mtandao usiotumia nyaya – wireless network wapo mbioni kuhakikisha ndoto ya kufanya vifaa vingi viwe na uwezo wa kuwasiliana vyenyewe kwa wenyewe. Hapo kabla ni computer tuu ndio ziliweza kufanya mawasiliano kwa internet,  lakini miaka ya hivi karibuni tumeshuhudia hata simu zikitumika kufanya mawasiliano kwa njia ya internet.

Nyuma ya pazia katika mawasiliano haya ya internet, kuna teknolojia zinazofanya tuweze kufanya mawasiliano haya – teknolojia ambazo zimepewa majina tofauti kuendana na toleo husika, na kila toleo la teknolojia ya wireless inaitwa Generation (kizazi) . 
Mfano kuna 1G (1st Generation), 2G ( 2nd Generation), 3G ( 3rd Generation), na hivi karibuni tumeshuhudia kuibuka kwa teknolojia yenye kasi zaidi ya 4G (4th Generation). 

Teknolojia ya 4G, huitwa pia LTE ( Long Term Evolution) ndio inayoelezwa kuwa tegemeo la kuifanya dunia iwe na mawasiliano ya kasi kubwa zaidi na kutokana na uwezo huo, basi vifaa vingi vitaweza kuunganishwa kupitia internet, kitu ambacho watabiri wanakiita “ Internet of Things”.

Zipo tayari simu zenye uwezo wa kuunganishwa na kasi hii ya ajabu ya 4G au LTE, na kama unawaza kununua smartphone, basi wahi fasta smartphone yenye uwezo wa 4G.

Nokia na Siemens kwa mfano wanatabiri kuwa vifaa vingi kama vile magari  na birika za kuchemshia maji/kahawa vitaunganishwa kwa internet. Jionee hapa video ya maelezo kwa ufupi kuhusu LTE:

Share:

0 comments:

Post a Comment