MAANA YA SEO NA MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA KUFANYA SEO

 

Maana ya SEO

SEO ni kifupi cha maneno ya kiingereza yafuatayo – Search Engine Optimization. Hata hivyo hiyo sio maana ya SEO. Tunaposema SEO tunamaanisha ni jumla ya maarifa yanayofanywa ili kufanya machapisho yapewe kipaumbele kwenye search engines kama vile Google, Yahoo, Bing n.k pale mtu anapokua anatafuta kitu kupitia search engines hizo. Katika makala hii, Mbuke Times, tutakuwezesha uelewe vema maana ya SEO na mambo gani uyazingatie unapofanya  SEO.

Jinsi SEO inavyofanya kazi

Kazi kubwa ya SEO ni kuhakikisha kuwa watu wanaposearch mtandaoni kitu fulani basi website/blog yako nayo ionekane kwenye ukurasa wa kwanza wa majibu ya search husika kwamba na wewe pia una kitu ambacho wao wanakitafuta.

Tuchukulie mfano kwa search engine ya Google. Unapoandika climb Kilimanjaro, utaletewa majibu mengi kutoka websites/blogs mbalimbali. Lengo la SEO ni kuhakikisha website/blog yako inakuwepo kwenye hayo majibu katika ukurasa wa kwanza.

Mambo ya kuzingatia ili kuifikia maana ya SEO

Ili ufahamu SEO inavyofanya kazi inakupasa kwanza ujue jinsi search engines kama vile Google , Bing n.k zinavyofanya kazi.

Kwanza kabisa, fahamu kuwa Search engines zina lengo kuu la kuwapatia watumiaji wa mtandao majibu bora ya kile wanachokitafuta mtandaoni.

Hivyo basi, ili search engines ziyape kipaumbele machapisho yako ni lazima kwanza yawe yenye ubora , yaani yenye kujibu haswa kile ambacho watu wanatafuta mtandaoni.

Pili elewa kuwa search engines huanza kwanza kukusanya machapisho kutoka katika websites na blogs na kuzihifadhi taarifa hizo ili pale mtu anapohitaji taarifa basi zenyewe huchunguza katika hifadhi zake kuona machapisho yapi yanaweza mfaa haswa mtu anayetafuta kitu husika.

Hii ina maana kuwa machapisho yako yanapaswa kuandaliwa kwa namna ambayo search engines zinaweza kuyakusanya kwa urahisi na kwa ubora zaidi. Mfano unapaswa kubainisha keyword phrase, kuwepo na picha, picha ziwe na ALT text , kuwe na subheadings n.k.  Tutayazungumzia hayo yote hapo baadae.

Tatu, search engines kama tulivyoona kuwa zinamlenga mtafutaji wa taarifa apate majibu bora. Njia nyingine wanayotumia kujua kuwa machapisho ni bora ni kwa namna machapisho “yanavyopigiwa debe” ya kuwa ni bora. Machapisho hupigiwa debe kwamba ni bora kwa namna ambavyo watu wengi wameshare. Search engines hutumia links toka websites na blogs mbalimbali kupima ubora wa machapisho yako. Hivyo ni vema kufanya juhudi ili websites na blogs mbalimbali ziweze kuchapisha au kulink website/blog yako.

Nne,  watu wengi siku hizi hutumia simu na tablets kuingia mtandaoni. Hivyo ili search engine ione kuwa machapisho yako yanawafaa wale wanaotafuta taarifa mtandaoni, inakupasa ujitahidi website yako iwe inamuonekano mzuri kwenye simu na tablets.  Kitaalamu tunasema website au blog yako iwe mobile friendly.

Hitimisho:

Usikose makala nyingine ambapo tutachambua zaidi kuhusu faida za kufanya SEO.

Kama unawaza kuanza kufikiria kufanya SEO, tuwasiliane sasa kwa namba +255 623 029 683 ili tukusaidie.

Share:

MAMBO YAKUFANYA KIPINDI HIKI CHA COVID-19 KAMA WEWE NI MJASIRIAMALI


coronavirus covid-19 na wajasiriamali

Tishio la ugonjwa wa virusi vya Corona  (COVID-19) ni kubwa sana. Tayari shirika la afya duniani (WHO) limetangaza kuwa COVID-19 ni janga la dunia. Athari za COVID-19 kwa biashara ni kubwa sana ikiwa ni pamoja na biashara nyingi kufungwa, wafanyakazi kupoteza ajira, wengine kupunguziwa mishahara na hata baadhi ya biashara kuanza kutangaza kufirisika. Katika makala hii tunakuelezea ni mambo gani unayoweza kufanya kama unamiliki biashara ili uweze kupita salama katika kipindi hiki kigumu.
Chukua tahadhari za kiafya zinazoshauriwa:
Uhai una thamani kubwa sana kuliko faida au biashara unayoihangaikia. Hivyo usihatarishe maisha yako kisa kutaka faida. Hapa tunamaanisha nawe mjasiriamali chukua tahadhari zote zinazoelekezwa katika kujilinda dhidi ya Coronavirus ikiwemo kuosha mikono  kwa maji yanayotiririka, kutopeana mikono na watu, kukaa mbali na watu wenye dalili za kuwa na COVID-19 na kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima.
Jenga brand yako:
Huu ndio wakati ambapo watu wengi watatumia mtandao iwe ni kwa simu au kwa kompyuta, hivyo ni wakati mzuri sana kwako mjasiriamali kuweka machapisho sio tuu yanayotangaza bidhaa au huduma yako bali yanayoweza kujenga brand yako, yaani machapisho yatakayoonyesha wewe ni mtu wa aina gani, biashara yako inaamini katika nini, na uguse hisia za watu kwa namna ya kipekee.
    
Jiandae kupunguza bei za bidhaa au huduma zako:
Huu ni wakati ambapo watu wengi hawatokua na kipato cha kutosha kufanya manunuzi kama walivyozoea. Wengine watakua wamekatwa mishahara, na wengine vyanzo vyao vya mapato vitakua vimekauka. Hivyo kupunguza bei ni namna ya kuwafanya wateja wako waweze kweli kufanya manunuzi.
Weka mipango ya kupunguza gharama za uendeshaji na malipo mengine mapema kabisa:
Kwakua hautopata mapato kama kipindi  kabla ya janga la Coronavirus , inakupasa ujipange sasa namna ya kupunguza gharama zako ili kwamba usishindwe kuzifanyia malipo. Njia za kupunguza gharama za uendeshaji zinaweza kuwa: Kufanyia kazi majumbani , kuacha matumizi ambayo sio ya lazima, kupunguza wafanyakazi, kupunguza mishahara, kuomba kuahirisha kufanya malipo fulani kama vile kuomba ulipe madeni baada ya miezi mitatu toka sasa n.k.
Weka mipango ya namna ya kukopa kwa unafuu
Kwakua kuna uwezekano utakosa mapato ya kutosha kutokana na hali ya kiuchumi kuwa ngumu , basi utakuja kuhitaji fedha za kuendesha biashara yako au hata kulipia marejesho ya mikopo yako ya zamani. Ni wakati sasa wa kuanza kufuatilia wapi unaweza pata fedha ya mkopo. Sio lazima ukope benki, waweza angalia vyanzo vingine kama vile watu binafsi au asasi nyingine zenye kutoa misaada kwa wajasiriamali.
Hitimisho:
Tuwasiliane kama unahitaji ushauri au namna ya kuwafikia wateja ili kuendelea kuboresha biashara yako. Tumia namba +255 623 029 683 tuwasiliane kwa WhatsApp au kwa namba ya kawaida.

Share:

JINSI YA KUINGIZA BIASHARA YAKO MTANDAONI



kufanya biashara mtandaoni

Katika ulimwengu wa kidigitali tulionao biashara yako inahitaji kuwa mtandaoni (online), lakini katika nyakati hizi za tishio la ugonjwa wa Coronavirus (COVID-19) sio tena swala la hiari kuwa mtandaoni bali kuwa mtandaoni kunageuka kuwa ni lazima kama unataka kuendelea bado kufanya biashara. Hii ni kwa sababu ya hali ya wasiwasi wa maumbukizo na marufuku ya kuwepo kwenye mikusanyiko ya watu wengi.
Fanya mambo yafuatayo ili nawe ufanye biashara kupitia mtandaoni:
1.Uwe na Website:
Unahitaji kuwa na sehemu moja mtandaoni ambapo watu watapata taarifa zote za msingi kuhusu biashara yako kwa namna ambapo zitakua zimepangiliwa vema. Sehemu hiyo ni website. Utakua na anuani ya website yako ambapo watu watapata kuingia kwa kupitia browsers kama vile Google Chrome, Internet Explorer , Mozilla Firefox n.k.  Unahitaji website hata kama unazo akaunti za social media kwakua website itatoa maelezo yote kuhusu website yako kwa namna bora zaidi kwani utapangilia taarifa zako vema, na pia ni sehemu rahisi ya kuanza kujenga uwezo wa watu kuifikia biashara yako hata wakiwa wanasearch mtandaoni.
2. Anza kuandika Blog:
Unahitaji kuandika mara kwa mara machapisho yatakayojibu changamoto na kuwapa wateja watarajiwa taarifa za msingi wanazohitaji. Hii itawafanya watu wawe karibu na biashara yako , waifahamu vema na bidhaa zako na mwisho wa siku watake kufanya biashara nawe.
Mfano unauza nguo, unaweza kuwa na blog inayozungumzia mavazi, fashion na namna ya kuwa na muonekano bora na mvuto. Watu watakaosoma blog yako watapendezwa na kujitoa kwako kuwasaidia na pia watajifunza kuhusu biashara yako inavyoweza kuwapatia mavazi na vitu vingine ili waweze kuwa vile ambavyo wewe umeelezea kuwa wanahitaji kuwa ili wawe na muonekano bora na wenye mvuto.
3. Wekeza kwenye kutumia Social Media kwa ubora zaidi
Haitoshi tuu kupost kuhusu bidhaa au huduma zako ukiwataka watu wanunue. Unahitaji kuwa ‘social’ yaani ujichanganye na jamii kwa kuwa na vitu tofauti tofauti vya kupost zaidi ya bidhaa. Utumie social media kama Facebook, Instagram, Twitter na WhatsApp kujenga brand yako ili uweze kuwa na uwezo haswa wa kushawishi watu kuhusu bidhaa au huduma zako. Pia social media ikusaidie kuwafanya watu watembelee website pamoja na blog yako.
Unaweza kuwa na magroup ya WhatsApp na Facebook ili uweze kuendelea kuwa karibu na wateja wako, ukiwaelimisha na kuwasaidia kujenga mtandao kati yao ili mwisho wa siku ujenge jamii (community) inayojumuika pamoja kupitia brand yako.

4. Lipia matangazo ya mtandaoni
Kulipia matangazo kama vile ya Facebook, Instagram , Google Ads na mengineyo ni muhimu sana haswa kwa ajili ya kupata watu wengi zaidi waone kile unachokitangaza kwa haraka. Hata hivyo usibweteke na matangazo hayo kuwa yatavuta watu na kujenga brand. Inakupasa uendelee kuwekeza kwenye kuelimisha, kuburudisha na kuwashirikisha watu wakuelewe kwa ukaribu zaidi na waipende biashara yako.

Hitimisho:
Umuhimu wa kufanya biashara mtandaoni una umuhimu mkubwa sana katika kipindi hiki, lakini ili ufaidike na mtandao unahitaji kujipanga vema katika kuingia mtandaoni. Sasa umeshajua mambo hayo makuu matatu ya kufanya ili uingie mtandaoni. Jibidiishe ufanye vema. Mtandao unalipa. Ukiwa na swali au unahitaji  tukusaidie kutekeleza na kusimamia mpango huo wa kuingia mtandaoni, tafadhali tuwasiliane kwa namba +255 623 029 683 kwa simu ya kawaida au kwa WhatsApp kwa namba hiyo hiyo.

Share:

MAMBO YA KUFAHAMU KUHUSU PRESENT CONTINUOUS TENSE

present continuous tense
''I am looking at you''. Mfano wa sentensi ya present continuous tense


Tenses katika Kiingereza ni muhimu sana kwani kutunga sentensi kunahitaji sana ujue upo kwenye tense ipi ili sentensi utakazotunga zilete maana unayokusudia. Kwa leo tuangalie mambo ya msingi kujua kuhusu Present Continuous Tense.  Katika kujifunza Present Continuous Tense na tense zote katika Kiingereza unapaswa kuzingatia haya tutakayosoma.

Utangulizi Kuhusu Present Continuous Tense:
Kwenye Kiswahili, tense hii ya Present Continuous Tense hutambulishwa na  kiashiria cha NA, mfano niNAkula, waNAimba, waNAlalamika. Kwa watu wengi tuzungumziapo Present Continuous Tense hufikiria tuu kuwa ni ile tense ambayo huonyesha matukio yanayoendelea wakati sentensi zake zikitajwa. Mfano nikisema I am singing – niNAimba, basi lazima niwe ninafanya hilo tukio la kuimba.
Hata hivyo tunapoenda kuangalia kazi za Present Continuous Tense, utaona kuwa tense hii ambayo kwa Kiswahili inatafsirika kama Wakati Uliopo Katika Hali ya Kuendelea ,  huwa ina kazi nyingi Zaidi ya kusema tuu tukio linaendelea.

Kazi za Present Continuous Tense:
Present Continuous Tense ina kazi zifuatazo:
1. Kuonyesha tukio linaendelea wakati sentensi inatajwa.
Mfano: I am teaching you now- Wakati huu nina kufundisha.
2. Kuonyesha mchakato wa tukio fulani unaendelea. Hii ina maana kuwa sio lazima kila tutumiapo Present Continuous tukio liwe linaendelea wakati sentensi inatajwa. Ila unaweza itumia Kama tukio lipo kwenye mchakato wa kufanyika.
Mfano : This year I'm helping people from Tanga - Haina maana kuwa wakati huu naongea ndio nawasaidia watu toka Tanga ila ninachomaanisha ni kuwa hilo swala la kuwasaidia watu ninalifanya.
3. Kazi ya tatu ya Present Continuous ni kuonyesha kuwa tukio fulani limeamuliwa kufanyika wakati ujao
Mfano: I am cooking rice tomorrow - (Nimeamua nitapika wali kesho).

Kutunga Sentensi za Kiingereza kwa kutumia Present Continuous Tense
Kutunga sentensi inapaswa ujue kuwa MATUKIO yote yawe na ING yaani kwa mfano go iwe going, eat iwe eating, play iwe playing.
Halafu utumie Auxiliary Verbs zifuatazo:
Kwa he, she na it tumia IS
Kwa they, we, you na I tumia ARE
Kwa I tumia AM
Mfano:
I am eating - Ninakula

She is eating- Anakula
We are eating – tunakula

Kuuliza Swali Katika Present Continuous Tense
Anza na Auxiliary Verbs Kisha mtendaji halafu tukio.

Mifano ya kuuliza maswali kwenye Present Continuous Tense:
(i) Je unapika ?
Mtendaji ni YOU, tukio Ni Cook na Auxiliary Verb ya YOU ni ARE hivyo itakua:
Are you cooking ?

(ii)Je wanaimba ?
Mtendaji ni wao - they, tukio ni Sing, na Auxiliary Verb ya they Ni Are hivyo itakua:
Are they singing ?

(iii)Je ninalia ?
Mtendaji Mimi -I , auxiliary verb ya I ni AM na tukio Ni Cry hivyo itakua
Am I crying ?

Kukanusha Katika Present Continuous Tense

Kukanusha katika Present Continuous Tense kufanyike kwa kutumia kanuni ifuatayo:
Mtendaji + Auxiliary Verb+ not + Verb

Mifano ya Kukanusha katika Present Continuous Tense :
(i) Mimi siimbi
I +am+no+ singing
Yaani I am not singing

(ii)Hatupiki
We are not cooking

HITIMISHO: Kama nilivyodokeza pale awali kuwa nyakati(tenses) katika English ni mada muhimu sana. Na natumaini katika Makala hii umepata mwanga wa mambo gani ya msingi ya kujua kwa kila aina ya tense utakayojifunza.
Ili ujifunze Zaidi kuhusu tenses, nakushauri ujipatie kitabu nilichoandika ninachochambua tenses zote kwa kina, na mifano kibao. Zaidi sana katika kitabu hicho utajifunza pia kuhusu Passive Voice, Conditional Sentences na Indirect Speech. Kitabu ni tshs. Elfu KUMI tuu. Tuwasiliane kwa WhatsApp 0623 029 683 ujipatie hicho kitabu.


Share:

JINSI YA KUSALIMIANA KATIKA ENGLISH


Salamu katika Kiingereza
Kusalimiana ni jambo la msingi sana katika lugha yoyote. Makala hii inakupa ufahamu kuhusu mambo ya msingi ya kufahamu na kuzingatia kuhusu kusalimia katika English. Utajifunza salamu katika kiingereza zipoje na jinsi ya kujibu.
Kwanza kabisa elewa kuwa LUGHA yoyote ni sehemu ya utamaduni wa wale wanaoitumia lugha hiyo. Hivyo basi kwakua tamaduni zipo tofauti ndivyo ilivyo hata kwenye matumizi ya lugha.
Mfano:
1.Kwenye English hakuna salamu maalum kwa mtu mzima au aliyekuzidi rika kama ilivyo kwa Kiswahili kuwa tuna SHIKAMOO kwa watu wazima au waliotuzidi rika.
Hivyo kwa mfano salamu ya GOOD MORNING (Gud moning) ambayo tafsiri yake ni ‘’ZA ASUBUHI” ni kwa watu wa marika yote. Hata HOW ARE YOU? ( Hau a yu ?) ambayo tafsiri yake ni ‘’U HALI GANI ?” ni kwa watu wa marika yote.
2. Kuna mazungumzo  katika Kiswahili  ambayo hayapo katika English. Mfano kwenye Kiswahili tunayo “Umeamkaje ?”, hatuna sentensi yenye tafsiri hii ya moja kwa moja katika English. Badala yake tumia HOW DID YOU SLEEP (Hau did yu slip?) ambayo ukiitafsiri moja kwa moja kwa Kiswahili itakua  ‘’ULILAJE?’’ila haifai kuitafsiri moja kwa moja.
3. Elewa kuwa kama ilivyo kwenye Kiswahili kua kuna aina ya salamu ambazo hutumika tuu kwa watu wa rika zako au watu wako wa karibu, hivyo hivyo kwenye English zipo salamu ambazo nazo ni za watu wa rika yako au watu wako wa karibu. Salamu hizi huitwa INFORMAL GREETINGS.
Tambua hata hivyo kuwa Informal Greetings za Kiswahili sio lazima zitafsirike moja kwa moja kwa English.
Mfano: Kwenye Kiswahili huwa tunasema MAMBO? kwenye English sema WHAT’S UP? (Wats ap?) ukiitafsiri moja kwa moja hiyo what’s up itamaanisha KIPI KIPO JUU?

Baada ya hayo tuangalie sasa salamu mbalimbali katika English.

KUSALIMIANA ASUBUHI:
Good morning ( Gud moning)  -  ZA ASUBUHI
Jibu: Good morning, how are you? (Gud moning, hau a yu?) -ZA ASUBUHI, UHALI GANI?
I am fine, thanks. How are you too? (Am fain, thenks, hau a y utu?)  - MZIMA , ASANTE. UHALI GANI NAWE? Au ingeweza kusemwa hivi:
I am fine, thanks.  How did you sleep ? (Am fain, thenks, hau did yu slip?)  MZIMA , ASANTE. UMEAMKAJE?
Ukiulizwa HOW DID YOU SLEEP? Jibu hivi :  GREAT ! (Gret) - (VIZURI SANA) au kama haujamka vema, basi NOT WELL (Not wel) kwamba  SIKUAMKA VIZURI.
Au kama unataka kuelezea kuwa mambo sio mazuri wala sio mabaya, ili mradi siku zinaenda unaweza sema.
I CAN’T COMPLAIN  ( I kent komplein) – SIWEZI LALAMIKA

KUSALIMIANA MCHANA
Kwa mchana waweza salimia hivi:
Good afternoon ( Gud aftanun) – HABARI YA MCHANA ?
Kuitikia: Good afternoon, how are you? ( Gud aftanun, haw are yu?) – HABARI YA MCHANA, WAENDELEAJE?
Kumbuka , katika English , hata kama mlikwisha salimiana asubuhi, bado mchana waweza kutumia salamu hiyo hiyo niliyoielezea hapo juu.

KUSALIMIANA USIKU
Good evening ( Gud ivining) – HABARI YA JIONI ?
Kuitikia: Good evening, how are you? ( Gud ivining, haw are yu?) – HABARI YA MCHANA, WAENDELEAJE?
I am fine, thanks. How are you too? (Aiem fain, thenks, hau a y utu?)  - MZIMA , ASANTE. UHALI GANI NAWE?
Jibu: I’m great , how was your day ? (Am gret, hau woz yua dei ?) – NIPO POA SANA,  JE SIKU YAKO ILIKUA VIPI ?
Jibu: It was great, thanks. ( It woz gret, thenks) – ILIKUA POA SANA , ASANTE

Kumbuka kusalimiana hata kama ni usiku tumia Good evening kama ilivyoelekezwa hapo juu. Ila kama ni kuagana au kumtamkia mtu usiku mwema ndio utumie GOOD NIGHT.

TUWASILIANE: Kwa masomo zaidi ya English tuwasiliane kwa WhatsApp 0623 029 683 au nipigie kwa namba hiyo hiyo tuzungumze zaidi namna gani nitakusaidia uweze English vema.

Share:

JINSI YA KUWA NA BLOG YA KULETA WATEJA WA BIDHAA AU HUDUMA YAKO

Hakuna biashara bila kuwa na wateja, na Hakuna mauzo kama wateja unaotarajia hawanunui bidhaa zako. Kama unajiuliza utafanyaje ili upate mauzo ya kutosha mtandaoni basi endelea kusoma hapa maana utagundua kanuni na mbinu ambazo zitakuwezesha kuongeza mauzo  ya bidhaa zako haswa kama unataka kufanya mauzo mtandaoni.
Usikose darasa maalum kuhusu blogs na biashara kwa undani zaidi na mada nyingine, ni jumapili hii Julai 16, kuanzia saa tatu usiku kupitia WhatsApp na FB. Tuwasiliane upate utaratibu wa kujiunga na darasa hilo..

Mtazamo sahihi kuhusu kuuza
Jiulize je mtu anaweza nunua basi kwa ajili ya kufanya biashara ya Dar hadi Zanzibar ? Au kununua meli kwa ajili ya kusafirisha mizigo kati ya Iringa na Mbeya? Bilas haka jibu ni hapana, hivyo hivyo mtu hawezi kukutafuta kwa bidhaa au huduma yako kama bidhaa au huduma yako haikidhi hitaji lake.
Kazi yako kuwa katika blog yako ni kuonyesha bidhaa au huduma yako inaweza kweli kukidhi mahitaji yake.

Jinsi ya kutangaza vema bidhaa au huduma zako kupitia blog yako mwenyewe
Kuna namna mbili ya kuelezea bidhaa zako kwa mteja. Moja ni njia ya moja kwa moja , na nyingini ni njia isiyo ya moja kwa moja ila mteja mlengwa ataweza kuunganisha ‘picha’ na kujua nini haswa unauza na kuelewa namna gani na  yeye anaweza kunufaika na huduma au bidhaa zako.
Njia ya moja kwa moja ya kutambulisha bidhaa na huduma zako kupitia blog yako
Hii ina maana ya kuelezea wazi wazi kupitia matangazo yako katika blog. Zaidi ya matangazo unaweza weka ukurasa maalum wa PRODUCTS au SERVICES halafu katika ukurasa huo ukaelezea hizo bidhaa zako.
Wengine hutumia pia ukurasa wa CONTACT US kuelezea kile wanachouza.
La msingi la kukumbuka ni kuwa watu hawaji kwa blog yako kusoma kuhusu bidhaa au huduma zako hivyo hakikisha haujazi blog yako kwa matangazo , au habari ya nini unauza.

Njia isiyo ya moja kwa moja ya kutambulisha bidhaa na huduma zako kupitia blog yako
Mfano mzuri wewe usomapo ujumbe huu tayari unaweza kupata picha aina gani ya huduma sisi tunatoa, nap engine bila hata kukuambia wewe mwenyewe unaweza kutaka kututafuta tukusaidie kuhusu blog yako au kuhusu mbinu za ujasiriamali na masoko. Kama umeliona hilo haujakosea kabisa, ndivyo ambavyo hata wewe ukiwa na blog na kuandika kwa umakini utaweza kueleza vema kuhusu bidhaa au huduma zako.
Njia isiyo ya moja kwa  moja ya kuelezea bidhaa na huduma zako kwa mteja, inahusika na wewe kama wewe kujionyesha kweli unajali yale wateja wako wanayopitia, hivyo unawaelezea nini kinaweza kuwatoa huko walipo. Kwakufanya hivyo utakua unatangaza huduma au bidhaa zako kwani bidhaa au huduma zako zinaweza kuondoa hayo ambayo watu wanakumbana nayo.
Sisi Mbuke Times mara zote hufanya hivyo na tunaona matokeo makubwa sana.
Mfano mzuri  ni vile ambavyo tumekua tukipokea wanafunzi wa kuwafundisha English kwakua wamesoma mbinu na miongozo mingi kuhusu English kutoka kwa blog yetu.

Weka wateja wako mbele kwanza
Fikiria yale wanayohitaji kufahamu na uandike kuhusu hayo kwa kuhusanisha na kile ambacho wewe unauza.
Fanya iwe rahisi watu kusoma blog yako, tumia vizuri rangi za background na rangi za maandishi. Tumia picha na vielelezo vingine Zaidi ili kweli unachoandika mtu akielewe.
Tumia muda kufanya utafiti wa unachoandika na pia utumie muda wa kutosha kutafakari na kupangilia mawazo yako ili unachoandika kivutie na kieleweke vema.
Wateja wako wataona jinsi unavyowajali kwakua muonekano wa blog yako na kile  unachoandika kitakuelezea wewe ni mtu wa aina gani haswa.

Namna ya wasomaji kuwasiliana nawe
Hakikisha blog yako imetaja wazi njia zipi ambazo wateja wako watarajiwa wanaweza

Jiandae kuuza kwa wale watakaotembelea blog yako
Blog sio sokoni kusema watu waje wanunue bidhaa au huduma zako. Blog ni mahali ambapo unatakiwa kuwafanya wale ambao sio wateja, wafikirie kuwa wateja. Itahitaji watu hao wasome Makala zako nyingi sana ili waweze kweli kujiridhisha na bidhaa au huduma zako, usijali hilo.
Kumbuka wapo watu wanaokuja kwa blog yako kwakua tuu walikuwa wanatafuta taarifa Fulani Fulani, hao sio kwamba wapo tayari kununua. Wanaweza kusoma blog yako na kuhifadhi jina la blog yako kwa ajili ya baadae watakapokuhitaji.
Kuna ambao watakuja kwa blog yako kwakua wapo tayari kununua. Hivyo ukikoleza maelezo yako vema na kuonyesha kweli wewe unaweza kuaminika , watu hao wanaweza kuja kukutafuta.
Kumbuka katika hali zote, mtu akikutafuta sio kwamba ndio tiketi kwako kuwa tayari mauzo yamekamilika. Unahitaji bado kuendelea kumuonyesha kwanini akuamini na kununua toka kwako.
Inakupasa uwe na lugha nzuri, uweze kutumia KANUNI ZOTE ZA MSINGI ZA KUFANYA MAUZO.

Call to Action zinahitajika katika blog
Je blog yako na Makala zako zina call to action? - yaani kile ambacho unataka watu wafanye kabla ya kuondoka hapo kwa blog yako ? Calls to actions inabidi ziwe na lugha nzuri na zijikite kwa mteja na kile anachoweza kupata toka kwako.

Fanya utafiti
Ni kweli kuwa watu wengi huandika blog kama hobby au kitu wakipendacho. Hata hivyo kumbuka hobby yako au ukipendacho sio  lazima kiwe ambacho watu wanahitaji au kinachoweza kukuingizia mapato ya kutosha.
Fanya utafiti kuhusu jamii na haswa wasomaji wako na fans wako kwenye mitandao ya kijamii. Utapata kujua nini haswa kinahitajika.

Sikiliza wasomaji wa blog yako
Soma comments, messages na emails toka kwa wasomaji wako. Utaweza kugundua nini haswa wanahitaji wewe uwaambie , na nini cha kuboresha. Hii pia itakufanya ujue namna gani bora Zaidi ya kutambulisha bidhaa na huduma zako kwao.
Mfano mzuri hata post hii unayosoma ni kwa sababu ya swali la mmoja wa wasomaji wangu aliyetaka kujua atafanyaje awe na blog inayomuingizia hela kupitia huduma zake kama mtaalamu wa mambo ya saikolojia. Mie nimeamua kuongeza zaidi ili jibu langu liwanufaishe watu wengi zaidi.

Umakini na ubora wa unachopost katika blog yako
Kazi kubwa ya blog katika kufanikisha mauzo ya bidhaa au huduma yako ni kujenga uelewa kuhusu nini unauza , kujenga uelewa wa wewe ni mtu wa namna gani, na Zaidi sana kujenga kuamini na kutegemewa na wale wanaosoma Makala zako.
Hivyo wekeza kweli kweli katika kile unachoandika kiasi kwamba atakayesoma apate picha ya juhudi na kazi uliyonayo katika kuwafikishia ujumbe na hivyo watu hao watategemea.
Kwahiyo ingawaje unahitajika kuandika Makala mara kwa mara, haina maana basi ndio ‘ulipue lipue’ ili mradi tuu uwe na Makala. Wasomaji wako wanajua kutambua Makala zilizoandikwa kwa umakini na kwa kujitoa kweli kweli, na zile Makala zilizoandikwa ili mradi tuu kutaka watu watembelee blog yako.
Ukiandika Makala kwa umakini na upendo mkubwa watu watataka pia kushare na hata wenye blog wengine watataka waweke kwa blog zao na kutaja wewe na blog yako hivyo kujijengea kufahamika Zaidi.

Search Engine Optimization
Unahitaji kuandika kwa umakini lakini pia kuandika kiasi kwamba search engines kama vile Google, Bing na Yahoo waweze kuzifikia Makala zako kwa urahisi na kuorodhesha Makala zako katika ukurasa wa mwanzo pale mtu anaposearch mtandaoni.
Search Engine Optimization inakuhitaji uangalie namna utumiavyo maneno yanayoweza kutafutwa mara kwa mara , pia ujue namna ya kuandika vichwa vya habari, picha zenye majina sahihi na maelezo mengine sahihi, pia Makala iwe na wingi unaofaa wa maneno sio tuu ka Makala kafupi ka aya moja.


Share:

FAIDA 5 ZA BLOG KWA MJASIRIAMALI


Kwa bahati mbaya wengi wakisikia blog hufikiria blog kama chombo cha kuandika habari za udaku au matukio fulani fulani  tuu ya kijamii.
Blog ni zaidi ya hivyo, blog ni moja ya nyenzo muhimu sana katika kujenga BRAND na kuongeza MAUZO ya bidhaa na huduma zako.
Unachotakiwa ni kufahamu vema jinsi ya kuandika blog kama mjasiriamali. Jikite katika shughuli au bidhaa unazouza, na ufahamu vema nani haswa walengwa wako.
Kuwa na blog yenye muonekano mzuri ni jambo la msingi , lakini sio kitu cha pekee unachohitaji kufanya.
Kama mjasiriamali unapaswa kutoa manufaa kwa wale unaowaandikia ili kweli wakutambue kuwa unaweza na wa kuamini. Nikudokeze tuu - moja ya misingi ya kuweza kuuza vizuri ni KUJENGA IMANI KWA WATEJA WATARAJIWA. Na hakuna sehemu nzuri ya kujenga kuaminika kama sio kupitia blog yako.
Wasiliana nasi tukutengenezee blog na website na kukuelemisha namna gani blog inaweza kuwa chombo cha kujenga biashara yako. WhatsApp 0757 120 020 au +57 301 297 1724.
Share:

TOFAUTI 4 KATI YA MJASIRIAMALI NA MFANYABIASHARA

Wengi wapo kwenye biashara hata hivyo hujiita wajasiriamali. Hii ni kwa sababu kumekua na mchanganyiko mkubwa kuhusu nani haswa ni mjasiriamali na nani mfanyabiashara.
Makala hii itakufanya usichanganye maneno hayo mawili, na ufahamu kama wewe ni mfanyabiashara au mjasiriamali na mwisho ni matumaini yetu Makala hii itakufanya uwe na hamu ya kuwa mjasiriamali badala ya kuwa mfanyabiashara.
Tutaanza kwanza kuangalia ufanano wa mjasiriamali na mfanyabiashara.
Mambo ambayo   mjasiriamali na mfanyabiashara wanafanana
  • Wote wawili hujikita katika kufikisha bidhaa au huduma fulani kwa walengwa wao. 
  • Wote wawili hufikiria manufaa wanayoweza kupata kutokana na hicho wanachokifanya.
  • Wote wawili wanaweza kunufaika kutokana na hicho wanachokifanya.
  • Mwisho wa siku wajasiriamali wengi na wafanyabiashara wote hujihusisha na biashara -yaani kuuza kitu fulani kwa faida.

Mambo ambayo mjasiriamali na mfanyabiashara wanatofautiana

Utofauti wa lengo kuu kati ya mjasiriamali na mfanyabiashara
Mjasiriamali ingawa anaweza kunufaika yeye kama yeye kutoka na anachofanya, lengo lake la msingi huwa sio yeye kama yeye afanikiwe, bali lengo lake ni kuona suluhu Fulani ya tatizo ambalo anataka kulitatua. Hivyo basi mjasiriamali hujikita Zaidi katika jamii, kuangalia nini anaweza kufanya cha kuleta ahueni. Mjasiriamali huhamasika zaidi na vile ambavyo anaweza kutatua changamoto fulani. Kwa upande wa mfanyabiashara lengo kuu ni kupata faida, hakuna mtazamo wa kina kuhusu changamoto gani au kwa namna gani jamii husika itapata haueni.  Ingawa anachofanya mfanyabiashara kinaweza kuleta ahueni na kutibu changamoto Fulani, lakini hilo sio wazo lake kuu au sio ambacho haswa kimemuingiza katika biashara. Yeye mfanyabiashara kinachompa hamasa kweli ni “kupiga hela” fasta.
Utofauti katika ubunifu kati ya mjasiriamali na mfanyabiashara
Mjasiriamali hujihusisha zaidi na kubuni bidhaa au huduma mpya au namna mpya ya kuwasilisha bidhaa na huduma zilizopo, au kufikia kwa namna ya kipekee soko jipya kwa bidhaa ambazo tayari zipo. Unaona katika kila jambo mjasiriamali hujihusisha na UPYA Fulani.  Kwa upande wa mfanyabiashara hujishughulisha na vitu ambavyo tayari vimekwisha buniwa bila kuongeza kitu cha ziada. Hii ni kwa sababu lengo la mfanyabiashara ni kufanya chochote kile kitakachomuingizia faida. Mfano kwakua kaona mwingine anauza nguo na zinatoka, basi yeye ataenda kununua nguo za aina ile auze tena kwa soko lile lile ambalo mwenzake anauza.
Mahusiano na watu wa karibu katika shughuli
Mjasiriamali kwakua ana lengo la kutengeneza kitu fulani na mtazamo wake upo katika jamii, mara nyingi hujikita katika kutafuta timu bora ya kufanya nayo kazi kwakua mjasiriamali ana mtazamo mpana wa kuona kitu alichonacho kinafikia mbali na anajua bila watu wazuri wakaribu yake hatoweza. Wakati huo mfanyabiashara kwakua hujikita zaidi katika kutafuta faida, na yeye mara nyingi manufaa yake binafsi ndio jambo la msingi zaidi, huwa hatilii maanani sana mambo ya mahusiano na kukua kwa pamoja na wale anaofanya nao shughuli yake. 
Mjasiriamali huboresha na kuzingatia hata mahusiano yake na mteja, na kwamba mteja na mfanyakazi ni sehemu muhimu ya biashara wakati kwa mfanyabiashara mteja ni mtu tuu wa pembeni wa nje ya biashara yake, na wafanyakazi kama tuu watoa huduma wa kumnufaisha yeye mfanyabiashara afikie malengo.
Hatari ya kupata hasara ilivyo kati ya mjasiriamali na mfanyabiashara
Kwakua mara nyingi mjasiriamali ni mwanzishaji wa bidhaa au huduma mpya au namna mpya ya kufikisha bidhaa au huduma iliyopo katika soko jipya au ambalo tayari lipo, mara nyingi mjasiriamali huwa hatari kubwa sana ya kupata hasara ukizingatia huo upya wa kufanya jambo.
Kwa upande wake mfanyabiashara ingawaje nae anaweza kupata hasara katika shughuli yake , hatari yake ya kupata hasira haiwezi linganishwa na mjasiriamali kwakua yeye mfanyabiashara anahusika na bidhaa au huduma ambayo tayari imekwishafahamika utaratibu wake wa jinsi ya kutengeneza na kuuza.  

Share:

TABIA 9 KATIKA KUTUMIA ENGLISH AMBAZO SI NZURI HATA KIDOGO

Kama unajifunza English au undataka kutumia vizuri English jitahidi sana utumie kanuni na taratibu sahihi za uandishi na uongeaji wa kiingereza. Katika makala hii fupi nitakukumbusha mambo 9 ambayo hutakiwi kuyafanya ili usionekane unatumia vibaya English.

Katika English kuna tabia sugu ambazo ni mbaya kweli kweli ngoja nizitaje hapa chini.
1. Kutokutumia alama za maandishi kwa usahihi. Mfano pa kuweka kiulizo usiweke kiulizo. Au kutumia alama ya kushangaa wakati huhitajiki kuitumia au kuzitumia nyingi bila sababu. Ushawahi ona mtu karibu kila aandikacho humalizia na !!!!!!!
2. Kutumia vifupi vya maneno isivyopaswa mfano Its Friday badala ya It's Friday
3. Kutokutumia herufi kubwa ipasavyo mfano tunasoma kuwa proper nouns zote ni lazima ziandikwe kwa herufi kubwa ila utakuta mtu kaandika jina lake au la mkoa kwa herufi ndogo
4. Kutokutumia maneno ya kuonyesha ustaarabu kama vile please, would, may, can. Usipotumia haya utajikuta ukionekana kama vile unatoa amri au sio mstaarabu.
5. Kuandika I kwa herufi ndogo mfano: John and i are friends.
6. Kutokutumia salamu kwa ufasaha kulingana na aina ya mtu unayewasiliana nae. Mfano hufai kumsalimia boss wako au mwalimu wako HEY!
7. Katika kuongea kuna ile tabia ya mtu kujilazimisha kuiga lafudhi kama vile ni mtu wa nchi fulani matokeo yake anasikika kama kero kwa huyo anayeongea nae. Jitahidi uongee taratibu na utamke maneno kwa ufasaha lakini sio utake kuonekana wewe kuwa ni mmarekani au mwingereza kwa mfano.
8. Kutokufanya punctuation ipasavyo mfano penye kutakiwa comma usiweke comma. Mfano mzuri katika picha hapa ya post hii DON'T TEACH JOHN ina maanisha usimfundishe mtu aitwaye John, waka Don't teach, John ina maana kuwa mtu aitwaye John ndio anaambiwe asifundishe.
9. Kutokufanya juhudi kuandika maneno ya English kama yanavyotakiwa kuandikwa badala yake kufanya mazoea ya kuandika English kama Kiswahili au kuiga maneno ya watu mfano Thanks kuandika TX.

Share: