JIFUNZE ENGLISH: JINSI YA KUSOMA SAA NA TAREHE KWA ENGLISH

kusoma_saa_English
Kusoma saa na kusoma tarehe kwa English ni muhimu sana kama sehemu ya wewe kujua English kwa ufasaha. Katika Makala hii tutajifunza vema namna tofauti za kusoma saa na kusoma tarehe kwa kiingereza.

Kusoma tarehe katika English:
Kwenye English tarehe huandikwa kwa kuanza na SIKU halafu MWEZI halafu mwaka. Mfano  16th  Feb. 2017, na utaisoma hivi : SIXTEENTH of February  Two Thousand and Seventeen.                        

Kumbuka: Kuna mbili za kusoma mwaka yaani

Kusoma namba nzima nzima  mfano: 2017 waweza sema namba kamili yaani elfu mbili na kumi na saba hivyo ukasema Two thousand and seventeen.
Njia ya pili ya kusoma mwaka ni kwa kusoma kwa mafungu ya namba mbili mbili yaani 20 halafu 17 hivyo ikawa TWENTY SEVENTEEN.

Kumbuka kwenye kutaja siku huwa tunasoma kwa viashiria hivi kutegemeana na namba ya mwisho ya tarehe:
1 – th yaani first mfano 1st Jan.2017 first of January twenty seventeen. Au 21st Jan 2016 ikasomwa Twenty first of January  twenty sixteen.

11 – th mfano 11th Feb . 2015 Eleventh of February twenty fifteen.
2 – nd mfano 2nd March 2016 Second of March twenty sixteen.
12- th mfano 12th April 2015 Twelfth of April twenty fifteen
3-rd mfano 3rd May 1998  Third of May nineteen nighty eight.
23 – 23rd  mfano 23rd June 2010 Twenty third of June twenty ten
Pia tambua kuwa kuandika tarehe inategemea na aina ya English, kama ni British English hiyo ambayo mnaitumia huko Tanzania ni kuwa unaanza na siku halafu mwezi halafu mwaka yaani 16th Feb. 2017 ila kama ni American English tarehe huandikwa kwa kuanza na mwezi kisha siku halafu mwaka yaani kwa mfano Feb . 16,2017 
                      
Jinsi ya kusoma saa kwa English                                                                       
Kuna namna mbili za kusoma saa katika English

Aina ya kwanza ya kusoma saa kwa English
Katika aina hii huwa tunaanza kutaja dakika kisha saa.  Na kumbuka katika English saa hutajwa kama mshale unavyoonyesha. Hivyo kwa mfano saa mbili asubuhi mshale utakua kwenye namba NANE, nawe utasema EIGHT usiseme kama kwa Kiswahili tunavyosema MBILI halafu ukasema TWO.
Mfano mweingine 7:25AM kwa Kiswahili ni saa moja kumi asubuhi ila kwa English kumbuka tunasoma saa kama zilivyoandikwa hivyo badala ya MOJA tutasema SEVEN. 
Kusoma dakika pia katika English kunategemea na je dakika zipo kabla ya 30 au baada ya 30 kama unavyoweza kuona katika picha hapa chini.
dakika_minutes_in_English

Hivyo kwa saa 7:25AM jiulize je dakika zipo kati ya dk 1 hadi 30 ? Kama ndio basi tumia PAST ukitaja dakika. Yaani mfano Twenty Five Minutes Past SEVEN.                                               

Tukumbuke AM maana yake ni kuanzia saa sita kamili usiku hadi saa tano na dk 59 asubuhi. Baada ya hapo ni PM    
                   
Aina ya Pili ya kusoma saa kwa English
Namna nyingine ya kusoma saa kwa English ni kwa kutaja namba kwa makundi mawili. Yaani kwanza kundi la saa kisha kundi la dakika. Mfano: 11:20 AM utasema Eleven Twenty in the morning                       Mfano mweinine 1:20PM utasema One twenty in the afternoon.                        


Hauna haja ya kusema ni afternoon au evening au night kama unaongea na mtu moja kwa  moja kwakua huyo mtu atakua akijua unataja saa gani kama unachotaka kusema wakati huo ni saa ngapi.
Angalia mfano hapa chini wa kusoma saa mbalimbali

Jifunze Zaidi:
Jiunge na group letu la WhatsApp kwa kutuma maombi ya kujiunga kwa namba hii +57 301 297 1724. Na pia karibu ujipatie kitabu chenye kanuni za msingi za kujua English. Kitabu kinaitwa English: Mbinu na Kanuni za Kuijua. Kitabu kinapatikana popote ulipo pale maana utatumiwa kwa email au kwa WhatsApp au kwa Facebook. Kitabu ni Tshs. Elfu Kumi na Tano.
kitabu_cha_English


Share:

1 comment:

  1. NIKUPONGEZE KWA MAELEZO MAZURI NA YAKUELEWEKA. ILA NINASWALI JE? NI KITU GANI HASA CHAKUZINGATIA KUSUDI KUWEZA KUONGEA MAANA IYO NDO CHANGAMMOTO KUBWA ASANTE.

    ReplyDelete