INAKUAJE MTU ANAWEZA KUANGALIA MOVIE NA KUTOKWA NA MACHOZI INGAWA ANAJUA WAZI SI KWELI?

Umewahi kuona au imekutokea wewe kuangalia Movie na ukajikuta machozi yanakutoka ? Au unaingiwa na HOFU kana kwamba na wewe umo katika movie.
Hii inakukumbusha kuwa hisia huweza kukufanya uamini jambo na hata udhani ukweli ndio huo kumbe kilichopo ni msukumo tuu wa hisia zako kuhusu kitu husika.
Na kama wanavyojifunza watu wanaotengeneza movie namna bora ya kujenga kitu chenye kubeba HISIA, usisahau wapo wengine wanaotumia MBINU HIYO YA HISIA, kukuaminisha mambo ambayo pengine sio sawa, pengine kwa akili ya kawaida usingeyakubali.
Upo uwezekano wa HISIA zako kutumiwa na mtu mwingine ku "take advantage of you " - sijui tuseme vipi kwa kiswahili -pengine neno sahihi la "take advantage of you" ni mtu kukufanya ufanye jambo kwa kutumia upenyo wa wema wako au kwa sababu wewe umeingia katika mtego waliouweka.
--Ingawaje inaweza kuwa ngumu kutumia AKILI mahali ambapo unatumia HISIA, naamini wewe kufahamu hili la kuwa HISIA zako zinaweza kutumika vibaya na mtu mwingine, kunaweza kukufanya uwe makini na maamuzi yako unayoyafanya kwa hisia.
--Maeneo ambapo HISIA zako zinaweza kutumika vibaya ni kama kwenye mapenzi, urafiki, dini na siasa. Hata hapa FB nimewahi kuona posts zikisema kama kweli wewe unapenda ...fanya hivi...Hii inalenga hisia zako kwani si kweli kuwa KUTOKUFANYA hicho wanachosema kunabadilisha lolote kuhusu UPENDO wako, au MSIMAMO wako kuhusu jambo fulani. 
N:B Hadithi ya hisia na movie ni kwa hisani ya Andy Hunt katika kitabu chake PROGRAMATIC THINKING AND LEARNING.
Share:

0 comments:

Post a Comment