IFAHAMU KANUNI HII ITUMIWAYO NA UBONGO WAKO

Ubongo wetu unatumia kanuni ya "KAMA KITU HAKITUMIKI BASI HAKINA UMUHIMU" hivyo huwa ngumu kwa ubongo kukupatia majibu kwa haraka kwa vitu ambavyo havijaonyeshwa umuhimu na wewe mwenyewe.
Kuelewa vizuri embu chukulia mfano rafiki zako mliosoma darasa moja shule ya msingi, pengine leo ukiulizwa uwataje hata 10 tuu kwa majina hukumbuki, ingawaje mlikuwa mkiitana majina kila siku wakati mlipokuwa shule na enzi hizo ulikumbuka bila shida.
--Ni kwa sababu haujaitumia mara kwa mara ndio maana ubongo haukuletei kumbukumbu.
--Hivyo kama unataka uwe na uwezo wa kufanya jambo fulani kwa ubora zaidi inakupasa uwe unafanya jambo husika mara kwa mara. 
Hivyo kama unataka kuwa mtu wa kufanya mambo ya busara, kutoa points unapozungumza basi fanyia kazi swala hilo.
Ndio maana hata leo ukiangalia mazoezi ya timu ya FC Barcelona bado wanafanya mazoezi ya kupiga pasi, na kumiliki mpira.
--Na kumbuka pia ubongo hauna uwezo wa kutambua lipi ni bora kwako, wenyewe unaangalia umuhimu wa kukumbuka kwa kadri unavyotumia kitu husika. Hivyo ndio maana wengine unakuta kati ya neno na neno wameweka TUSI, kwakuwa ndio wamekwisha zoea hivyo. Ukijizoesha kusoma udaku na kufikiri udaku basi hayo ndio ubongo wako utakumbuka.
Kwa mujibu wa Brainworldmagazine.com na Lifehack.com
Share:

1 comment: