HIVI NDIVYO ELIMU YAKO ITAKAVYOKUSAIDIA KUPATA KAZI (TAFAKARI)

Kuna wakati unaweza kusikia mtu akilalamika kuwa amefuata MAELEKEZO yote aliyopewa ili kufikia lengo fulani lakini hakufanikiwa. 
Katika hali hii kutokufanikiwa kunaweza kutokana na:
1. Maelekezo yenyewe inawezekana hayakuwa sahihi.
2. Ulifuata maelekezo kwa usahihi kabisa ila uliyafuata kwa tafsiri yako isiyo sahihi.
3. Mazingira yamebadilika hivyo pamoja na kufuata kwa usahihi na kwamba maelekezo kweli yalikuwa sahihi, lakini mazingira/nyakati haikuwa sahihi.
4. Pengine unahitaji tu uvumilivu kidogo kwani matokeo yanaweza kuchelewa.
Unganisha post hii na maisha ya kila siku. Wengi wanamaliza vyuo kisha kubaki mtaani wakiwa hawana kazi, pengine walisoma kweli kwa umakini na kupata alama nzuri hivyo wanataraji kupata kazi haraka iwezekanavyo. Hata hivyo jiulize:-
**Je elimu uliyopata ni sahihi kufanikisha upate kazi kiurahisi -je unao ujuzi kweli, je unaweza kujieleza?
**Mazingira ya kupata kazi yamekuwa tofauti na yataendelea kubadilika siku hadi siku, je elimu yako imekuandaa kupambana katika mazingira tofauti au inakupa tuu cheti ?
**Pengine ulielewa vibaya kuhusu ELIMU, wakati ule unapiga CHABO, na kuibia ukijipa imani kuwa la msingi ni CHETI tuu, labda hapo ndipo ulipotafsiri vibaya kuhusu ELIMU, ila leo unalalamika iweje haupati kazi au michongo mingine ingawaje una ELIMU.
Share:

0 comments:

Post a Comment