HII NDIO TEKNOHAMA: KWANINI HAITOSHI TUU KUJUA KUPOST, KUCOMMENT NA KUCHAT FB ?

Wapo wengi wanaoendesha magari na hawajui hata jinsi gari linavyofanya kazi zaidi ya kujua jinsi tuu ya kuendesha gari. Lakini hata kama haujui nini kinafanyika mpaka gari liongeze mwendo au kufunga breki, bado unahitajika kujua namna bora ya kutumia vioo vya pembeni, kioo cha kuangalia nyuma, matumizi sahihi ya taa-kama ni "full" au dim, na zaidi unahitaji kujua jinsi ya kufunga breki,kuongeza mwendo na kurudi nyuma ("RIVASI"). --
Hali hii ni tofauti kwa hapa MTANDAONI sio tuu kwamba unatakiwa kujua namna ya kuitumia TEKNOHAMA bali ili kuwa salama na kuepuka wewe KUTUMIKA isivyopaswa na wenye kuijua TEKNOHAMA , unahitaji kujua namna TEKNOHAMA inavyofanya kazi. 
Mfano: Wengi wanachojua khs FB ni kuwa unaingia unasoma posts za watu, unapost picha na status zako basi. Lakini haujui namna ambavyo taarifa zako za hapa FB zinavyoweza kufika mikononi mwa watu usiotarajia. Je, wajua kwa mfano unaweza chagua nani aone POSTS zako na nani asione? Je, wajua kuchagua nani anaweza tuma maombi ya kuwa rafiki yako hapa FB ? Je, wajua namna ya kuzuia taarifa zako zisitumiwe na FB kwa matangazo ? Je, wajua kuwa FB inafuatila mwenendo wako mtandaoni ili kupata kufahamu zaidi kuhusu wewe, na je kama hautaki unazuia vipi? 

Kama unajua programming, basi ni rahisi kwako kuelewa kwanini ni rahisi kwa FB kufanya hivyo wanavyofanya. 

Na kama umesoma lugha kama JavaScript na PHP utajua mambo mengi ambayo wenye kuendesha websites wanafanya juu yetu bila sisi kujijua.

N:B Soma kwa umakini hiyo habari kwani kuna walioielewa tofauti kama huyu fan wa ukurasa wetu
FAN ANASEMA: Mie nafahamu vizuri. Ila kwa mambo ya security kwenye post zako,friend requests na hata advertisement nadhani FB wenyewe wanatoa hiyo huduma sidhani kama mpaka ujue programming ndo uelewe hizo huduma. Na sidhani kama normal end user ana ulazima sana wa kujua hivo vitu labda awe exceptional kama mie na wewe tunavyofahamu programming na web languages pamoja na security scripting mfano hiyo javascript. Ni mgawanyo tu wa knowledge mbalimbali.

JIBU LANGU NI: Post haijasema MPAKA UJUE PROGRAMMING ndio UELEWE. Post inasema Kama unajua programming basi ITAKUWA RAHISI, kuelewa KWANINI NI RAHISI kwa FB kufanya hivyo. Na wala Post haijahusisha UELEWA WA PROGRAMMING na KUJUA HUDUMA ZA FB.
Na elewa kuwa ninapozungumzia kufahamu teknohama sio lazima kuwa mtu wa fani husika yaani wote tuwe programmers, hata kuwa tuu na uelewa kuwa hizi websites zinaendeshwaje, nao ni ufahamu mzuri katika kumsaidia mtu Kuwa na MATUMIZI BORA, sio kwamba bila hizo ELIMU hatoweza. Mfano mie ni MHASIBU na kazi zangu nyingi ni za MARKETING na UHASIBU, hata hivyo ufahamu wa TEKNOHAMA unaniwezesha kufanya mengi katika zama hizi za digitali  
Share:

0 comments:

Post a Comment