UTAPENDA KUSOMA STATUS HIZI 10 ZA FACEBOOK

Ndio, Facebook ni sehemu ambayo unaweza kuburudika na pia kujifunza mambo kadhaa ya kimaisha. Nakualika upitie status hizi za Facebook ujifunze kitu:-

Status 1:
Find X, in :- X+Y=18, given that Y=5.
Hapo GIVEN imerahisisha kazi.
Ingekuwa hivi hata ktk maisha kwani kuna vitu vingi GIVEN, ila bado tunaumiza vichwa. Mfano:-
----Ipo GIVEN kuwa: Sio kila mtu atapenda kila unachoandika hapa FB, ila mtu anaporopoka kwa kukukejeli, anakuwa "Amekuharibia Siku".
--Ipo GIVEN kuwa ni ngumu kujua ya ndani ya moyo/akili ya mtu, hata hivyo huwa tuna "maindi" pale best wetu anapotusema vibaya kwa watu wengine.

Status 2:
 Ajabu ila ni Kweli:
Mtu anataka Tanzania iendelee, pengine anaota iwe kama 'ulaya' lakini mtu huyo huyo ni mwingi wa Fitina, Majungu na Chuki kwa waTanzania wenzake wanaofanya uzalishaji/ubunifu wa kimaendeleo. Tena chuki, majungu na fitina hizo zinaelekezwa hata kwa watu wa UKOO wake!
---Ni sisi wananchi ndio wa kuleta maendeleo, serikali huweka mfumo, miundo mbinu, au mazingira bora kwa yetu.
----‪#‎MaendeleoHayaletwiNaWanasiasaPekee‬.

Status 3:
MUDA a.k.a WAKATI a.k.a TIME, ni mojawapo ya sababu kubwa ya utofauti wa viwango vya ubora wa maisha tulivyonavyo.
Wengine kila wiki au kila mwezi ukiacha kuingiza "Mshiko" wameingiza ufahamu fulani mpya, ufahamu wenye maana.Sio tuu wanawaza, bali wanaongeza uwezo wao wa baadae wa Ufanisi.
Ila kibongo bongo, wengi mpango mzima ni "mshiko" kwanza kwa sasa, kwa mbinu zile zile zisizobadilika+kucopy & paste.
Niingize kidhungu: I think TIME should be recognized as an Element of Production.
‪#‎Hatua3mbele5nyuma‬

Status 4:
Jambo La Kushare leo kuhusu AMERICA:
Nilipokuwa Afrika, hususani Tanzania tulizoea kuwaita watu toka USA kuwa ndio WAMAREKANI - yaani watu wa AMERICA.
Hata hivyo ukiwa bara la America wamarekani wanatambulika kama watu toka UNITED STATES, full stop. Kwani hata wa brazil nao ni waAMERICA, hata waColombia nao ni WaAMERICA.
--Hivyo kibusara mtu toka U.S.A hujitambulisha kuwa " I am from united States". Hamalizii lile neno AMERICA kwani watamshushua kuwa hata wao ni Wa AMERICA.

Status 5:
Mojawapo ya tatizo kubwa katika jamii zetu ni UGUMU WA WATU KUACHA WALIYOJIFUNZA, sio KUJIFUNZA MAPYA.
“The first problem for us all, men and women, is not to learn, but to unlearn.”
Gloria Steinem

Status 6:
There is really too little we can do Without Sacrifice.
Great things require great sacrifices.
Mambo Mengi ya Msingi Yanataka kujinyima, kutoa kafara !

Status 7:
One day, your ship will come in. Maybe it already has. But you will breakthrough and earn the money - and likely more - than you've always wanted. This will bring you many benefits, but a few problems as well, particularly in the form of negative reactions from others. No one will ever know how hard you worked to get where you are. No one will ever understand the sacrifices you made. It's not worth trying to explain.
----Craig Ballantyne

Status 8:
 KWA WENZANGU NA MIE MNAOJAZA ALAMA ZA RELI (#) KWENYE STATUS ZENU:
Kwa usahihi, alama ya # hutumika kuifanya status iingie katika kundi maalum la aina ya status. Mfano kama utaweka ‪#‎Majanga‬, basi unailazimisha status yako iingizwe katika kundi la status zinazotumia hiyo alama ya Majanga. Hii ina maana kuwa kama kuna watu wengine wametumia hiyo alama ya #Majanga, basi nyote status zenu zitaorodheshwa huko.

Status 9:

Mafanikio ya mtu yana mahusiano makubwa na ya moja kwa moja na namna anavyofikiri kuhusu makosa. Mfano kama umetia juhudi hasa za kutosha katika jambo kisha halikuwa vile ulivyotegemea, basi ujue huko si kushindwa, unajiweka sawa, wakati mwingine utaweza. Usiangalie nani alitegemea ufanye nini, wewe unajua uwezo wako ulipoishia, na dhamira yako ilivyokuwa safi katika hilo ulilolifanya. Unapojipa nafasi za kujaribu bila kuogopa kushindwa, na unapochukulia ushindi kama sehemu tuu ya maisha na mwanzo wa changamoto zingine, basi unajiweka vema kuwa 'mpiganaji' hodari na mtu mwenye mafanikio endelevu.
Tafakari....... Chukua Hatua.

Status 10:
Kipimo sahihi cha Maendeleo au Mafanikio yako sio kujilinganisha na wengine kwani siku zote watakuwepo watu waliokuzidi na unaowazidi. La Msingi ni kupima namna gani ulichonacho kinakusaidia kutimiza mahitaji na kukuweza kuuishi UBINADAMU wa kweli. Pengine, ukicheki ulivyoyapata hayo mafanikio waweza jisuta au kujipongeza vizuri !
N:B: Status hizo hapo juu ni kutoka kwa Facebook Profile yangu.
John.
Share:

1 comment: