USHAURI WA P.DIDY NA LIL WAYNE KWA WATAFUTAJI KAMA WEWE

Mara nyingi tumejikuta tukitamani kujua ‘siri’ ya mafanikio, au kanuni maalum ya kufuata ili tufanikiwa. Na kuna nyakati tumejikuta tukitamani kuiga wale tunaowaona wamefanikiwa ingawaje kiukweli hatufahamu kwa undani nini wamefanya kufikia hapo walipofikia.
Katika video hapo chini, utajifunza kuwa mara nyingi tunapoona mafanikio ya watu tukatamani kuwa kama wao , na tukajikuta tunaiga mambo fulani fulani ili kujiweka kama hao watu, pengine kuna kitu tunakosea kwani mara tunasahau, kuna mambo mengi ya ziada nyuma ya pazia hatuyajui kuhusu watu tunaojaribu kuwaiga, au tunaotamani kuwa kama wao.
La msingi P.Diddy na Lil Wayne wanasema ni kujitahidi kufanya kazi kwa bidii kwa kadri ya uwezo, usiige watu wengine, na jitahidi kuishi wewe kama wewe. Ina maana ni lazima kama unataka mafanikio endelevu, kwanza ujitambue, utambue nini unataka katika maisha yako, kisha utafute mbinu za kipekee na za uhakika za kufikia huko unakotaka kufikia. Zaidi sana usisahau bidii katika kujishughulisha ili kufanikiwa, hii inajumuisha kusoma sana ili kuongeza maarifa ya ujuzi wako, na kuwa mbunifu bila kuchoka.
Haya ni baadhi ya maneno katika video hii utakayoiona hapa chini:-

"Literally you just have to be really into what you are doing and what you are saying. You have to live it.... You don't have to try to be different, because when you try to be different, you all end up being the same because every body is trying to be different.
But you know what you got to do is be YOU, and if that doesn't work, then you know that is not what you should be doing”.

Share:

0 comments:

Post a Comment