PATA THAMANI YA FEDHA YAKO KWA KUTEMBELEA WEBSITES HIZI

Je, wewe ni mmoja wa watumiaji wa mtandao lakini haujaona bado mchango chanya wa mtandao katika kubadilisha na kuboresha maisha yako? Je, kwako internet ni sehemu ya ‘kupoteza muda’ tuu au ‘kuuza sura’?. Je, kwako mtandao ni sehemu ya kuingia kujua fulani kafanya nini, au usalimie tuu rafiki zako? Je, mtandao kwako ni sehemu ya kufanya tuu kazi ulizotumwa na bosi au assignments za chuoni ?.
Umefika wakati wewe mwenyewe uchukue utawala wa maisha yako, kwa kuhakikisha una ufahamu wa kutosha wa mambo kadha wa kadha yanayokuzunguka, bila kungoja kusikia kwa watu wengine au kufuata maoni tuu ya walio soma au kusikia mambo fulani huko mtaani. Mafanikio binafsi katika karne hii ya 21 yanategemea sana aina gani ya taarifa au ufahamu unao, na namna unavyotumia ufahamu husika.
Na kwakuwa imekuwa rahisi sana kutengeneza habari/taarifa mbalimbali, ni muhimu kwako kujua vyanzo vingi tofauti vya taarifa ili uwe na uhakika wa taarifa, isitoshe inabidi ufanye maamuzi sahihi ya vyanzo gani vya taarifa utavitumia katika kujifunza mambo mbalimbali.
Katika makala hii tunaonyesha vyanzo  saba ambavyo unaweza kutumia kupata ufahamu wa kuboresha maisha yako ya kishule, kijasiriamali, kikazi, na hata kimapenzi.

1. Videos:

Tumia videos mbalimbali zinazopatikana mtandaoni kupitia YouTube, TED, na, Vimeo, kujifunza mambo ya msingi. Waweza fanya hivi kwa kutembelea tuu website hizo au ukiwa kwa website hizo uka search kwa kuandika topic husika. Waweza pia tembelea WISE GEEK, huko unaweza pata majibu ya maswali mengi pamoja na Video za mada husika.

2. Kozi za bure:

Waweza jiandikisha online kwa kozi mbalimbali zitolewazo bure kabisa. Baadhi ya website unazoweza kutumia ni kama COURSERA, ALISON, STANFORD ONLINE, MIT OPEN COURSEWARE, na CLASSCENTRAL.
Kutoka katika website hizi utapata kujiandikisha katika vyuo vikubwa duniani kama Stanford, Duke, MIT, na kuhudhuria kozi mbalimbali ziwe za Saikolojia, Computer Science, Ujasiriamali, au hata Hesabu. Kama unapenda kupata vyeti, basi hakikisha unahitimu kozi husika, na utatumiwa cheti toka kwa chuo husika ulichojiandikisha.

3.Websites maalum : 

Kuna websites na blog kadhaa zenye makala maalum zenye uzito wa kimantiki katika kukusaidia kukua kifikra, kijasiriamali na kielimu. Website kama vile Big Think, Early To Rise, MattMorris, Mashable, Freeman Perspective, Casey Daily Dispatch, ni baadhi ya websites ambazo zinaibua mitazamo mipya ya kiteknolojia, kifikra, na kijasiriamali.

4.Google na Yahoo Alerts:

Tumia huduma hizi kupata habari zenye uzito wa kipekee kwako. Unachofanya ni kuenda kwenye website husika mfano Google Alerts, kisha unaorodhesha aina ya taarifa unazozitaka kupata. Kisha kupitia email uliyoiweka katika huduma husika, utakuwa ukitumia updates.

5.Subscribe:  

Tembelea mitandao mbalimbali yenye habari za kujenga, jisajili kupata taarifa toka kwao au kupata vitabu vya bure kutoka kwao. Mfano mzuri, kama unataka taarifa za marketing basi tembelea Hub spot na unaweza kujisajili kupata taarifa kibao, pamoja na vitabu vizuri sana vya mambo ya content marketing.

6.Mitandao ya kijamii:

Mitandao ya kijamii hususani Facebook inaweza kutumika pia kupata taarifa za kujenga.  Unachotakiwa kufanya ni ku LIKE kurasa zenye kusambaza taarifa za kukujenga, kisha utakuwa ukipata updates toka kurasa husika.  Ku LIKE pekee haitoshi, pia tembelea mara kwa mara kurasa husika ili kuona mambo mapya yaliyopostiwa huko. Kwani jinsi mitandao ya kijamii inavyooendeshwa, inawezakana isiwe rahisi kuona kila updates toka kwa kurasa ulizo LIKE. Ukiwa kwenye mitandao ya kijamii waweza jifunza lunga mfano Spanish kupitia ukurasa wa SpanishDict .

7. Hifadhi za nyaraka mbalimbali:

Tembelea websites kama vile Slide share, Prezi, Edocr na Scribd ambazo zinahifadhi makala mbalimbali ambazo watu wameandaa na kuziweka humo. Baadhi ya makala hizo unaweza ku download bure mtandaoni.
Share:

4 comments:

  1. Ahsante sana binafsi nimepata jambo hapa.

    ReplyDelete
  2. http://make-it-simply-easy-life.com/

    ReplyDelete
  3. The actual time and effort took to create this wonderful article were really great and would like to read this blog regularly to get more updates...
    AngularJS Training in Chennai | Devops Online Training

    ReplyDelete