HII NI KWA WAJASIRIAMALI WA SASA NA WATARAJIWA. Part 2

Leo tunaendelea na makala yetu ya mambo ya msingi kwa kila mjasiriamali kuyatilia maanani ili kuweza kuwa na mafanikio endelevu. Elewa tunaposema mafanikio endelevu tunamaanisha kuwa ni zaidi tuu ya kupata wateja leo, na kesho, bali uwezo wa kuendeleza biashara kwa miaka mingi kwakuwa mjasiriamali anaweza kumudu changamoto na matatizo yanayojitokeza katika fani hii ya ujasiriamali. Tuangalie sasa points zilizobaki , yaani 6-11:-

6. Kujenga Mtandao sahihi na kuutumia
Tunasema kujenga mtandao sahihi na kuutumia, na sio tuu kuwa na mtandao wa watu wasio na tija kwako kwakuwa pengine hawana cha kukupatia, au wewe mwenyewe hauna maono ya jinsi ya kuutumia mtandao wako. Chunguza vizuri mtandao wako unaweza kukuta wapo wateja wako watarajiwa, wapo watu wanaoweza kukuuzia bidhaa, wapo watu wanaoweza kukupa ushauri bora wa kiundeshaji, wapo watu wanaoweza kukusaidia kifedha au hata watu wanaoweza kukuunganisha na watu wengine ambao watakuwa na tija kwako. Ni kweli kuwa hakuna mtu ‘asiye wa umuhimu’, unatakiwa kuwaheshimu watu wote, lakini pia ujue jinsi ya kutenda kazi zako na watu ili hata wale wanaoonekana kuwa ‘sio wa muhimu’ waonekane wa muhimu. Hata hivyo waepuke wale wanaokurudisha nyuma au wanaoweza kukurudisha nyuma.

7. Mahusiano na wateja
Biashara yako ni sehemu ya maisha yako, basi hata wateja nao ni sehemu ya maisha yako na ya biashara yako, hivyo ni muhimu kuweka mahusiano yenye tija na wateja husika.  Mahusiano ya wateja yanaanza kabla hata hajanunua bidhaa toka kwako, iwe kupitia utafiti wako wa soko – kutambua kwa undani mambo ya msingi yanayoweza kukufanya uuze bidhaa yako. Mahusiano yanaendelea pale mteja anapokuja kununua bidhaa kwako, na hayaishi  tuu hapo anaponunua bidhaa bali yanaendelea kwani ukiboresha mahusiano yako na mteja , anaweza kurudi tena kununua bidhaa toka kwako atakapohitaji, au anaweza kuwaambia watu wengine. Lakini pia mahusiano mazuri na wateja yanakuwezesha kujua namna unavyotakiwa kuboresha shughuli zako pamoja na bidhaa zako. Hivyo jifunze kusikiliza kwa ufasaha malalamiko ya wateja na kuyafanyia kazi, jitahidi kufuatilia taarifa zinazokuwezesha kujua hisia zao kuhusu biashara yako. Katika kujenga mahusiano bora na wateja, ni muhimu basi kuwa na mfumo mzuri wa kukusanya na kutumia taarifa zinazohusu mwenendo wa wateja wako. Kuna program maalum za kompyuta zinazokuwezesha kukusanya taarifa za wateja, hata hivyo waweza fuatilia mitandao ya kijamii kama Facebook ili kutambua tabia, mabadiliko na mitazamo ya wateja wako. Weka wazi mifumo ya kuwasiliana na wateja wako, mfano wateja waweze wasiliana nawe kwa barua pepe, simu, kuonana ana kwa ana, au hata kwa kuweka maoni yao katika kisanduku cha maoni.

8. Mahusiano na wanaokuuzia bidhaa/huduma
Unajenga mahusiano bora na wanaokuuzia bidhaa au huduma ili  kupata manufaa ya punguzo la bei, kuweza kukopeshwa bidhaa baadae,  na pia kuweza kutambua mabadiliko au maboresho kwa upande wa wanaokuuzia bidhaa /huduma  ambapo mabadiliko au maboresho hayo yanaweza kuathiri uendeshaji wa shughuli za biashara yako. Mfano, chukulia kampuni X unayoitegemea kwa ajili ya kupatia bidhaa fulani ambazo wewe huwa unauza , mara ghafla unapata taarifa kuwa imesitisha utengenezaji wa bidhaa zake, hivyo kujikuta wewe una athirika kwani ulikuwa unatarajia kupata bidhaa hizo toka kwake, na haukuwa umejipanga kifedha kununua kwa kampuni nyingne ambayo kwa kawaida huuza bidhaa kwa bei ya juu zaidi.  Laiti kama ungekuwa unafuatilia taarifa za kampuni husika unayoitegemea , ungekuwa tayari umejipanga iwe kununua kwa muuzaji mwingine kwa bei ya juu, au hata kufanya utafiti wa kutosha wa sehemu nyingine ya kununua bidhaa husika kwa bei nafuu.

9. Makubaliano /mikataba
Kuna mikataba au makubaliano kadhaa ambayo mjasiriamali utakutana nayo kama vile makubaliano na watu unaotaka kushirikiana nao kuanzisha biashara, makubaliano na wateja wako, makubaliano na wafanyakazi, makubaliano na wanaokuuzia bidhaa/huduma n.k.  La msingi hapa ukumbuke kulinda maslahi yako, na uhakikishe unaelewa vema vipengele vyote vya makubaliano, na ikibidi makubaliano hayo yawe katika maandishi na yashuhudiwe na mwanasheria. Hakikisha mfano wewe na washirika wako wa biashara mnakubaliana kuhusu mgawanyo wa majukumu yenu, jinsi mtakavyogawana faida, jinsi mtakavyo suluhisha migongano mbalimbali, jinsi mtakavyochangia mtaji wa biashara na namna ya mfumo wa uongozi wa biashara yenu.  Wengi huacha kuweka mikataba kwa kuwa tuu eti wanaaminiana. Kama wewe ni mmoja wao unaofikiria hivyo, tambua kuwa mkataba sio kwa sababu ya kutoaminiana, bali ni namna ya kuweka msisitizo wa kuelewana kwenu, na pia mnataka mambo yenu yaende vema, na inapotokea kutokuenda sawa, basi muwe na pa kuanzia katika kutafakari  jinsi ya kuboresha mambo yenu.

10. Utafiti
Kabla ya kufanya maamuzi ya msingi katika biashara yako kama vile kuajiri wafanyakazi wapya, kununua mashine mpya, kuzalisha bidhaa au huduma mpya, ni muhimu  sana kuwa na uchambuzi usio na mashaka unaotetea maamuzi yako ya kufanya hivyo unavyotaka kufanya.  Uchambuzi huo ndio tunaouita utafiti. Fanya utafiti kuhusu mfanyakazi unayetaka kumuajiri – mfano kupitia interview, kuwasiliana na waajiri wake wa awali, kutafuta historia ya maisha ya mfanyakazi mtarajiwa n.k. Hii itakuwezesha kujua kweli mfanyakazi au wafanyakazi unaoajiri kweli wataweza kutimiza yale unayokusudia wafanye. Hali kadhalika, unapotaka kufanya shughuli za kimasoko, inabidi ufanye utafiti ili kutambua kama kweli shughuli hizo zitaendana na hali ya soko, na kama kweli zitaleta tija kwako. Kumbuka rasilimali ulizonazo ni chache , hivyo ni muhimu uwe na nidhamu katika kuzitumia, na njia mojawapo ya kuwa na nidhamu ni kufanya utafiti kama kweli matumizi yako ya rasilimali yataleta tija. Utafiti sio lazima uwe wa gharama kubwa, waweza fanya utafiti kwa kusoma tuu makala na habari mbalimbali toka vyanzo tofauti, au kwa kuongea na wateja/wafanyakazi.

11. Usimamizi wa taarifa
Wataalamu wanasema katika ulimwengu wa teknolojia tulio nao sasa, mafanikio ya biashara yanachangiwa  na aina bora ya taarifa ambazo wamiliki/watendaji wa biashara wanazo, na ambazo wanaweza kuzitumia. Taarifa hizi ni kama vile mwenendo wa wateja, mwenendo wa wafanyakazi, mwenendo wa washindani wa biashara, mwenendo wa mabadiliko ya teknolojia, mabadiliko ya kijamii, na kisiasa n.k. Mjasiriamali inabidi uwe na uwezo wa kuendana na wakati kwa kupata na kutumia taarifa sahihi ili usiachwe nyuma na washindani wako, au wateja wasikukumbie kwakuwa haukidhi mabadiliko wanayoyahitaji.
Share:

1 comment:


  1. WELCOME TO THE GREAT BROTHERHOOD.
    Do you want to be a member of Illuminati as a brotherhood
    that will make you rich and famous in the world and have
    power to control people in the high place in the worldwide
    .Are you a business man or woman,artist, political,
    musician, student, do you want to be rich, famous, powerful
    in life, join the Illuminati brotherhood cult today and get
    instant rich sum of. 2 million dollars in a week, and a free
    home.any where you choose to live in this world
    BENEFITS GIVEN TO NEW MEMBERS of ILLUMINATI.
    1. A Cash Reward of USD $500,000 USD
    2. A New Sleek Dream CAR valued at USD $300,000 USD
    3.A Dream House bought in the country of your own choice
    4. One Month holiday (fully paid) to your dream tourist
    destination.
    5.One year Golf Membership package
    6.A V.I.P treatment in all Airports in the World 7.A total
    Lifestyle change 8.Access to Bohemian Grove
    account every month as a member
    9.One Month booked Appointment with Top 5 world
    Leaders and Top 5 Celebrities in the World.
    If you are interested of joining us in the great brotherhood of illuminati CONTACT MR ROLAND or WhatsApp him +2348142587627
    or email:illuminatipower666brotherhood@gmail.com

    ReplyDelete