UKWELI KUHUSU RANKING ZA FIFA


Umewahi kujiuliza jinsi ambavyo timu zinapanda na kushuka kwenye rank za timu bora za FIFA ? Basi tulia na ujisomee ufafanuzi uliotulia kabisa. Mambo ya msingi ya haraka haraka kufahamu kuhusu FIFA Ranking ni rank (nafasi) huchanganuliwa kwa mahesabu maalum ambayo hufanywa kila mwezi. 
Hivyo basi matokeo ya nafasi hizo hutolewa kila mwezi.

Na ujue pia kuwa hata timu ishinde Mechi vipi, sio kwamba ndio kigezo pekee kwa nchi kupanda nafasi. FIFA wanacheki pia na hizo timu unazozifunga zipo katika rank gani, umuhimu wa mechi, na historia yako kwa ujumla kwa miezi 48 iliyopita (miaka 4). Hivyo sio tuu Mmeshinda vimechi viwili vitatu basi mnataka muwe kwenye 2O bora.
 

Hivyo basi utaweza kujionea kuwa pamoja na kutolewa kwenye robo fainali ya AFCON 2013 IVORY COAST ndio timu namba 1 Afrika (ya 12 duniani),ikifuatiwa na GHANA (ya pili Afrika na ya 19 duniani), iliyotolewa kwenye Nusu Fainali.
Mali imekuwa ya Tatu kwa Afrika na ya 25 duniani wakati Mabingwa wa Africa Nigeria wameshika nafasi ya 30 duniani na kwa afrika nafasi ya 4.
 

Nchi yetu Tanzania  imeporomoka kwa nafasi 3 toka nafasi ya 130 duniani hadi nafasi ya 127. Kwa matokeo haya ya Februari 2013, Tanzania imekuwa ya 36 kwa ubora Afrika kwa kupanda nafasi 6 toka nafasi ya 42 iliyokuwa inashirikia mwezi Januari 2013.

Nafasi 10 bora kwa Afrika ni kama ifuatavyo:-


-----Kwa mujibu wa The FIFA/Coca-cola World Ranking kwa mwezi huu wa Feb.2013. Iliyotelewa Feb.14, 2013.
Share:

0 comments:

Post a Comment