MAANA HALISI YA KULA BATA

Kila kukicha tunaona mitandaoni au mitaani watu wakizungumzia 'kula bata'. Je, ni kweli kula bata ndio uthibitisho wa mafanikio ya kimaisha ? Je, kula bata ni sawa na kupumzika na kuburudika ? Je, ni kweli kuna maana tofauti za kula bata ?
Msikilize kijana huyu wa kibongo akielezea jinsi alivyo na maendeleo na anavyo kula bata !

“Mie, aah we acha kabisa, Mungu kanijalia neema, nina laptop, nina blackberry, nina badilisha club ninavyotaka, hizo Lounge ndio usiseme sijui Savannah, Nyumbani Lounge , huko kote mie nyumbani. 
Yaani mademu wanavyo ni shobokea, halafu mie hata si wamandai, nimepoa zangu na mademu watatu tuu. 
Yaani swaga ninazotoa Facebook, nina rafiki kibao, nakaribia kufikisha elfu nne. Mie si mkali bwana.

Dunia hii raha ujipe mwenyewe. Nijipe shida ya nini, wakati nakaa kwa wazee (wazazi), halafu naingiza kitu kama elfu ishirini kila siku. 
Kwani nikitumia elfu 15 kwa siku, ikabaki  5 inalinda mfuko, hata ikibaki buku ya vocha poa tuu, kuna shida gani?. Hela utumiavyo, ndivyo zinavyokuzoea”.


Kama kujipa raha kwenyewe ndio hivi, basi kazi ipo ! Maisha bora kwa kila mtanzania kweli yanawezekana!

Je, wewe maana yako ya kula bata ni ipi ?

Picha: via freephoto.com 
Share:

2 comments:

  1. Nimefika hapa kupata maanaya "kula bata" lakini naona maswali tu.

    ReplyDelete
  2. Nimefika hapa kupata maanaya "kula bata" lakini naona maswali tu.

    ReplyDelete