SIFA ZA KUWA MBONGO MZAMIAJI HUKO UGHAIBUNI

Kwa watu wengi , mpango wa kuishi nje ya nchi una maana ya ‘Kuzamia’. Yawezekana neno kuzamia linatumika sivyo ndivyo kwani asili yake ilikuwa haswa miaka ya nyuma sana , ambapo wengi walienda  nje ya Tanzania kwa kupitia meli ambapo walijificha baada ya kuzamia meli, na kuondoka na meli husika mpaka huko ughaibuni ambako wakifika huko hujichanganya na wenyeji na kuanza ‘kutafuta’ maisha. 
Pengine mtindo huu wa kuenda ughaibuni kwa kuzamia meli unatumika bado ila haujashamiri sana siku za hivi karibuni.

Badala ya kuondoka kwa mtindo huu wa kuzamia meli ambapo wazamiaji hao hawakuwa na hata vibali halali vya kuingia nchi husika, achilia mbali kuwa na hata Passport ya Tanzania, siku hizi, wabongo hawatumii meli kuzamia,  ‘wazamiaji’ wengi wa siku hizi huwa na vibali halali vya kusafiria na hata kupanda ndege au mabasi halali kabisa na kuingia nchi husika hata hivyo wanapofika huko hupitiliza muda halali wa kukaa huko nchi husika, na hivyo hiyo kuonekana kama na wao ‘walizamia’.

Kwahiyo neno kuzamia siku hizi halitumiki kama zamani kueleza taswira ya aina ya usafiri mtu aliotumia kusafiria – yaani kuzamia meli, badala yake neno kuzamia limekumbwa na utata wa maana tofauti. Kwa wengine neno ‘kuzamia’ linamaanisha aina yoyote ile ya kuishi ughaibuni zaidi ya shughuli halali iliyompeleka mtu kwa mara ya kwanza. 

Katika maana hii ya pili , kuna mgongano mwingine wa maana ya kuzamia. Je, wewe unaonaje:
1. Je  kila mtu anayeishi ughaibuni zaidi ya shughuli yake ya awali iliyompeleka huko ni mzamiaji hata kama anacho kibali halali cha kuishi huko ?

2. Au mzamiaji ni yule mbongo anayeishi ughaibuni pasipo kuwa na kibali halali cha kuishi huko ughaibuni ?
Share:

1 comment: