TAFAKARI MAKINI LEO: UMEISIKIA HII KITU KUHUSU "FUTURE" YAKO ?

Kama umewahi kuwa kiti cha mbele cha gari wakati wa usiku wewe kama dereva au abiria utakumbuka kuwa pamoja na taa za gari kuwashwa, mwanga wake haufiki mbali kumulika njia yote, bali humulika hatua chache hapo mbele.
Hata hivyo hali hiyo ya kutoona mbele haizuii kufika mwisho wa safari yenu.
 
Je, iweje leo wewe uache kujishughulisha na mambo ya yatakayoboresha maisha yako, kisa tuu ni kuwa eti hauoni kama kweli hapo mbele utafanikiwa ?
Kumbuka hauihitaji kuona wazi wazi mafanikio yako yatakavyokuwa hapo baadae, la msingi ni 


JE UNAFANYA LILILO SAHIHI ? JE, UNAJITUMA VYA KUTOSHA ? 

JE, UNAENDELEA KUJIFUNZA SIKU HADI SIKU ILI KUBORESHA SAFARI YAKO YA MAFANIKIO?
 

Kama unahitaji kuanza shule anza, kama unahitaji kuanza biashara anza, kama unahitaji kuanza kuboresha chochote kile anza leo, usisite kwa kuwa eti mafanikio hayapo wazi.
Na kumbuka hata kama hautofanikiwa, bado utakuwa umejifunza kitu na utaweza kuboresha safari yako.
 

--Ndio maana MBUKE TIMES inaendelea ingawaje nina ndoto tuu ipo siku itakuwa kitu kikubwa, ila kiukweli kwa sasa sina "picha halisi" itakuaje hapo baadae !
 

Mfano huu wa taa za gari ni kwa nukuu toka kwa E.L. Doctorow aliyelinganisha taa za gari na uandishi wa vitabu vya hadithi.
Share:

0 comments:

Post a Comment