FUNDISHO AMBALO KILA MJASIRIAMALI ANAPASWA KULIJUA

Wengi wanaweza kuanzisha biashara , hata hivyo ni wachache wanaweza kuendeleza biashara na hata kuwa na biashara zenye kukua na zenye faida.
Kuna mambo ukiyafahamu yanaweza kukusaidia kuwa mjasiriamali endelevu. Mambo hayo yanafanana na kuushinda mchezo wa MAZE.
Mchezo huo kama unavyoona pichani hapa chini ni kuwa unapewa njia ya kuingilia , na unaonyeshwa pa kutokea , hata hivyo utafikaje fikaje toka ulipoingia hiyo ni kazi yako kujua.
Ndivyo ilivyo katika ujasiriamali. Unapokuwa na wazo la biashara na malengo ya kuyafika mafanikio ya aina fulani. Unajua kuwa unaweza kuanza biashara husika, hata hivyo kuna mengi utakayokutana nayo kabla haujaipata njia ya mafanikio.
Ni kama ulivyo mchezo huu kuna njia nyingine ni rahisi tuu kuzipita, ila kuna nyingine unakutana na kuta ambazo inabidi uzivunje ili utokee sehemu nyingine.

Ni kweli pia unaweza kutumia muda mwingi sana na ukafanikiwa kupata njia ya kutokea salama kabisa katika mchezo huu wa MAZE, na ndivyo ilivyo hata katika ulimwengu wa ujasiriamali. Kuna wanaochukua miaka na miaka kufikia mafanikio yao, na kuna ambao hata hawafiki mbali wanakumbana na vikwazo na hawaoni njia ya kutokea.

Unafanyaje kupita salama mpaka mafanikio katika ujasiriamali ?

1. Elewa wazi kuwa ujasiriamali ni safari, sio jambo la mara moja tuu ufanikiwe halafu basi, uanze 'kula bata'. Ujasiriamali ni maisha, ni changamoto za kila siku na hivyo kubali aina hiyo ya maisha. Usiweke mbele sana wazo la kupata faida kwa haraka, maana utakata tamaa pale unapokumbana na vizuizi, wakati kama ulivyo mchezo huu wa MAZE, vizuizi ni sehemu tuu ya mchezo, ila kuna njia ya kufika.

2. Kazi yako kubwa kama mjasiriamali basi ni kutambua kwa haraka, tena kwa mtazamo wa juu vizuizi au changamoto unazoweza kukutana nazo, panga mikakati ya kutatua changamoto hizo. Kuna vizuizi vingine ni rahisi sana kama vile kuamua tuu kubadili njia, na kuna vingine ni lazima tuu uvishinde ili utokee upande wa pili. Kuvishinda vizuizi hivyo wakati mwingine si wewe peke yako unaweza. Unahitaji maelekezo na huduma za wataalamu, unahitaji fedha n.k

3. Kwa ujasiriamali endelevu ni lazima ujizoeshe kujisomea sana, na uweze kuwa na uwezo wa kuwa na watu wenye ujuzi wa kutatua matatizo.
Share:

0 comments:

Post a Comment