SOMO ZITO KUHUSU HATUA ZA KUWA MBUNIFU

Ubunifu na uthubutu wa kudadisi ni moja ya nguzo kuu za maendeleo na mafanikio ya mtu binafsi na hata mataifa. Rais Barack Obama ananukuliwa na website ya White House, akisema:
"The first step in winning the future is encouraging American innovation...... What we can do -- what America does better than anyone else -- is spark the creativity and imagination of our people. "
Ambapo twaweza tafsiri maneno hapo juu kama ifuatavyo:
"Hatua ya kwanza katika kuwa washindi hapo baadae ni kuhamasisha ubunifu wa Kimarekani....Kile tunachoweza kufanya --Kile ambacho Marekani inaweza kufanya kwa ubora zaidi zaidi ya wengine- yaani kuchochea ubunifu na udadisi wa watu wetu"
 Ubunifu unaleta faida kwa mtu binafsi kama vile:-
  • Kuweza kukabiliana na changamoto na ugumu wa kimaisha
  • Kuweza kuona nafasi za ziada za kuboresha maisha -"opportunities", kwani kiasili hatutengenezi "opportunities" bali tayari opportunities zipo, ila tunachofanya ni kuzitambua, na kuanza kuzitumia.
Kwa jamii kwa ujumla, Ubunifu husaidia:-
  • Kuweza kusaidia watu wengine
  • Kuweza kuongeza bidhaa na huduma kwa jamii
  • Kusaidia jamii kukabiliana na changamoto zilizopo
Makala hii inachambua kwa kifupi jinsi ya kuwa mbunifu. Haijalishi ubunifu ni wa namna gani - iwe kuandika kitabu, kuzalisha vyakula, kutoa huduma za ufundi n.k , yote hayo yanaweza kufanyika kwa ubunifu na kuleta manufaa.

Zingatia hatua zifuatazo:-

1. Jifunze kulikubali tatizo kama changamoto na fursa ya kuleta suluhisho: Wapo wengi ambao wanapoona ugumu katika jambo fulani, wanasita kuendelea au wanasubiri suluhisho toka kwa wengine. Ni kweli kuna mambo utawaachia wengine, lakini lile 'lililo karibu' na uwezo wako waweza litatua. Mfano ukaribu ninaozungumzia hapa inawezekana ni mazingira unayoishi, aina ya ujuzi wako, na uwezo wako

2. Tumia muda wa kutosha kujifunza: Ili kuwa mbunifu inakupasa uwe na taarifa za kutosha kuhusu tatizo unalotaka kutatua, ujue pia wengine wamefanya nini. Kujifunza ndio kunakopelekea uzoefu, na uzoefu au kubobea katika kitu ndiko kunakoleta ubunifu. Kumbuka kujifunza sio lazima uende darasani, waweza jifunza kwa kuona, kusikia, kujisomea, au kwa kufundishwa-darasani au sehemu nyingine yoyote ile.
Ndio maana STEVE JOBS aliwahi kusema :-
“Creativity is just connecting things. When you ask creative people how they did something, they feel a little guilty because they didn’t really do it, they just saw something. It seemed obvious to them after a while. That’s because they were able to connect experiences they’ve had and synthesize new things. And the reason they were able to do that was that they’ve had more experiences or they have thought more about their experiences than other people". 
Twaweza kutafsiri hivi:
"Ubunifu ni namna tuu ya kuunganisha vitu. Ukiwauliza watu wabunifu waliwezaje kufikia walivyofanya, wanajisikia hatia kwakuwa kiukweli hawakufanya lolote, bali waliona tuu kitu fulani. Ilionekana wazi kwao baada ya muda fulani. Hiyo ni kwa sababu waliweza kuunganisha uzoefu waliokuwa nao, na kuweka vitu kwa pamoja.Na sababu ya wao kuweza kufanya hivyo ni kuwa walikuwa na uzoefu, au walitumia muda mwingi zaidi kufikiria kuliko watu wengine, kuhusu uzoefu wao".
3. Thubutu Kuota: Baada ya kulitambua tatizo, ukawa tayari kulitatu, ukajawa na hamasa ya kujifunza, na ukajifunza vya kutosha kuhusu hali husika, kinachofuata ni wewe sasa kufikiria suluhu ya tatizo husika. Unachopasa sasa ni kupendekeza njia tofauti ya kufanya jambo, aina mpya ya bidhaa au huduma, na kujaribu hicho unachofikiria ili kilete mafanikio. Katika hali hii, Usiogope kukosea, na wala usiogope kuwa kitu chako kitakataliwa au kuonekana cha ajabu mbele ya watu wengine. Kwani kiuhalisi, ni kweli ni kitu tofauti hivyo jinsi watu wengine watakavyokipokea itakuwa tofauti.
Ndio maana Albert Eistein aliwahi kusema:-
"If at first, the idea is not absurd, then there is no hope for it".
Yaani: 
"Kama wazo, mwanzoni halionekani kuwa ni wazo la ajabu ajabu, basi hakuna matumaini juu yake".
Share:

1 comment: